Mkurugenzi wa Kituo cha Redio Jamii cha Tumbatu Ali Khamis Mtwana akimpatia maelezo juu ya utendaji wa Kituo hicho Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif mara baada ya kukizindua rasmi.Kulia ya Balozi Seif ni Mwakilishi wa Unesco Bwana Abdullwahabi Koribaly na Waziri wa Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo Mh. Said Ali Mbaouk.
Mkurugenzi wa Kituo cha Redio Jamii cha Tumbatu Ali Khamis Mtwana akifanya vitu vyake wakati akiwa hewani kurusha matangazo ya kituo cha Redio Jamii Tumbatu mara baada ya kuzinduliwa na Balozi Seif.
Mwakilishi wa Jumuiya ya Elimu, Sayansi na Mawasiliano ya Umoja wa Mataifa { Unesco } Bwana Abdullwahabi Koribaly akitoa salamu zake katika hafla ya ufunguzi wa kituo cha redio jamii Tumbatu kilichopata msaada na ufadhili mkubwa kutoka Jumuiya hiyo.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akizungumza na wananchi wa Kisiwa cha Tumbatu katika hafla ya uzinduzi wa Kituo cha Matangazo ya Redio Jamii Kisiwani humo.(Picha na Hassan Issa wa – OMPR – ZNZ).
No comments:
Post a Comment