Habari za Punde

Taarifa fupi ya Zacadia




Ndugu Wazanzibari, ndugu wageni wetu kutoka nchi mbali mbali, mabibi na mabwana, vijana  na watoto wetu.

Asalaam alaikoum warahamatu Allaah wabarakatuh (Meaning Peace be upon to you all.
We equally feel honored  to welcome our guests ,brothers , sisters and friends from other communities who took their precious time to come out  and support us tonight in this good cause  - we do say  thank you  very much.  Asanteni  sana !
We hope you will continue to repeat the same in the near future. Also please feel free to give us your ideas, opinions and any other valuable inputs or contributions. We are all proud to be part of this great Canadian society.Your support is very important to us and to those whom we are trying to help back home in Zanzibar, Tanzania.

Baada ya kutoa salamu, sina budi kuwakaribisha na kuwapa shukrani kwa kuupokea na kuitikia wito huu adhimu wa kuhudhuria katika mwaliko huu wa kuchangia watoto wetu mayatima na wengine  wengi sana wasio jiweza  huko visiwani Zanzibar na kusaidia hali mbaya ya uchumi na maendeleo ya nchi yetu Zanzibar .


Kama tunavyojuwa wengi wetu, kwamba serikali ya Zanzibar, baada ya kukaa na kutafakari na kugundua kuwa  nchi nyingi sana  duniani  zimefanikiwa kwa kiasi kikubwa mno kutoka kwa wanachi wake wanaoishi nchi za nje (Diaspora populations ) kwa kusaidia kuingiza mamilioni ya fedha, misaada, utaalamu wao, foreign invetsments  na kuanzisha biashara katika nchi zao za asili au kuzaliwa, kuukuza uchumi wa nchi hizo na kunyayua hali za maisha ya wanachi wao masikni na wasiojiweza  kwa kupunguza kiwango cha hali ya  juu cha umaskini na ufukara,  ndio Serikali ya Zanzibar ikaona iko haja ya kuiga mfano huo  na kutoa wito wa  kuwashirikisha Wazanzibari waishio nje ya Zanzibar ili kufaidika na  mbinu hiyo na hivyo ikaamua kuanzisha kitengo maaluum ndani ya ofisi ya Rais wa Zanzibar  ili kuchangia maendeleo ya “Uchumi  na Jamii,” ya nchi yetu ya Zanzibari  na watu wake.

Hivyo basi, baada ya serikali kuunda kitengo hicho kwa jina la “ Diaposra Desk” chini ya  Ofisi ya Rais ya Wizara ya Nchi na Ushirikiano wa Kimaifa Zanzibar, ilitoa wito kwa Wazanzibari walioko nchi za nje kujikusanya na kuandaa mikakati itakayoweza kutumika kuipatia misaada Zanzibar moja kwa moja, aidha kwa kushirikiana na taasisi  nyengine za ndani ya Zanzibar au kwa kushirikiana na serikali kwa baadhi ya sekta kubwa kubwa za uwekezaji.

Hapa Canada wito huo ulipokewa na baadhi ya Wazanzibari waliokuwa tayari kulifanyia kazi suala hili, walianza harakati za kujikusanya na kuunda chombo ambacho kitawawakiliha wana Diaspora wa Wazanzibari nchini Canada  na mwaka 2010 kikaanzishwa  chombo chetu hiki  huru  kinachojitwala wenyewe ambacho kinajulikana kwa jina la “Zanzibar-Canadian Diaspora Association” kwa kifupi ZACADIA na kupata usajili kwa jina la ZACADIA Foundation mnamo tarehe 12 April, 2012.

Nini Zanzibar Canadian Diaspora Association?:  Maana na Maumbile yake :Diaspora ni watu au raia wanaoishi  au kukulia nje ya nchi yao ya kuzaliwa au ya asili.  Kwa maana hiyo Zacadia ni outward looking International Organization” na lengo lake kuu ni kujenga Daraja litalounganisha mataifa mawili ya  Zanzibar na Canada  kwa maslahi ya kuleta maendeleo ya kichumi na kijamii kwa  mashirikiano ya Wazanzibari wa ndani ya Zanzibar  na wale wanaoishi Canada. Kwa maana hiyo  mfano tofauti na Zancana ambayo ni  inward looking local national organization” na lengo lake kuu ni kuwasaidia Wazanzibari katika masula ya ukaazi ya hapa Canada. Juu ya hivyo organizations zote hizi mbili  zinachukua uhuru wa kuwasaidia Wazanzibari  popote pale walipo mathalan  Zancana  kuwasaidia  vile vile Wazanzibari wanoishi Zanzibar ili kuonesha uzalendo kwa nchi yao na Zacadia vile vile tokea kuundwa kwake, mbali na yale malengo yake mama ya kuisaidia nyumbani Zanzibar katika sekta ya “ kunyayua uchumi na jamii yetu ,” pia juhudi kubwa imefanywa kuwasaidia Wazanzibari waishio ndani ya Canada  katika kupata wepesi wa baadhi ya masuala yao muhimu ya kiukaazi na uhamiaji .

Mpaka sasa kuna mambo mengi ambayo Zacadia imeyafanya ili kufikia lengo lake lakini  si rahisi kuyataja hapa  yote lakini baadhi yake ni haya yafuatayo :

1.       ZACADIA imeweza kusaidiana na Benki ya Watu wa Zanzibar katika kutafuta taasisi ya huduma za fedha ili kuweza kupata unafuu wa gharama za kutuma pesa Zanzibar. WorldRemit ni kampuni ambayo imekubali kushirikiana na PBZ katika kuwasaidia Wazanzibari kuweza kutuma pesa wakiwa ndani ya majumba yao kwa njia ya :online banking.

2.       ZACADIA imeweza kuwasiliana na PBZ ili kukubali kwa wale ambao watahitaji kufungua account zao katika PBZ na kuikubali ithbati ya ZACADIA kwa kuwagongea muhuri wa ZACADIA katika fomu zao

3.       ZACADIA imeshauriana na PBZ kuandaa fomu maalum za wana Diaspora badala ya zile ambazo ziko sasa na ambazo hazilingani na mazingira yetu ya huku Canada.

4.       ZACADIA imeweza kushirikiana na PBZ na WorldRemit katika kuweza kuwarahisishia Wanaoishi nje kuweza kutumia huduma za “online banking” ili waweze kufuatilia account na kuona harakati za account zao wakiwa huku Canada.

5.       ZACADIA  ikiongozwa na Board of Trustees na CEO wake , imeshaunda structure yake hapa Canada, na Zanzibar.  Kulingana na mahitaji ya nchi yetu Idara kadhaa za Zacadia zimeanzishwa zikisimamaiwa na Managers wake zikiwemo : Education, Health and Community Safety, Business, Investment and Banking, Women and Seniors,Youth and Children, Trade and Tourism, Fundraising and Resource Development, Spiritual Affairs, Treasury  and Administration. 

6.       ZACADIA tayari imeanza  kupeleka misaada mbali mbali ya wanaohitaji kama vile nguo, vyombo vya nyumbani, baiskeli, mapipa ya kuhifadhia maji na hata pesa taslim, kupitia mmoja wa manager wake amabye anasimamia wanawake na wazee huko Zanzibar, picha na video za ugawaji wa misaada hiyo zitaoneshwa leo hapa.

7.       ZACADIA imeshaandaa mradi wa watoto mayatima ambao una lengo la kuwatafutia watoto hao wadhamini watakaowashughulikia kwa huduma za elimu, afya, chakula bora na hata kuweza kuwasaidia wazee wao kwa kuwapatia huduma muhimu kama vile vyakula na kuwaelimisha namna ya kujienedeleza kwa kujitayarishia bustani zitakazoweza kuwapatia mahitaji yao madogo madogo.

8.       Tukiwa leo hii tuko hapa, ZACADIA inashughulikia kupeleka vitanda vya wagonjwa katika hospitali zinazohitaji sana, na tayari vitano vinatarajiwa kufika katika kituo cha afya cha Kiwani huko Pemba.

9.        Pia, tumeanza kuanzisha mashirikiano (patnerships)  na Jumuia mbali mbali za kijamii zilizoanzishwa huko Zanzibar katika kuifanyia utafiti miradi ambayo inahitaji kipau mbele katika kushughulikiwa na kufanya kazi pamoja

10.    Zacadia imeashaonana na vile vile kufanya uhusiano na mazungumzo na  mashirika kadhaa na tumeahidiwa ushirikiano na misaada mabali mbali  ili kutimiza malengo yetu. Mashirika haya yakiwemo East African Chamber of Commerce of Canada, Rotary Club, Islamic Relief Organization,Youth Challenge International, Zanzibar Diaspora Association of America (ZADIA)  Fisabililah, wabunge, Zanzibar Ministries of Education, Ministry of Health, Business and Commerce, Zanzibar Investment Promotion (ZIPA), Zanzibar Insurance, Peoples Bank of Zanzibar, Zanzibar Trade and Tourism, Zanzibar Social Security Fund, Zanzibar Institute of Research and Policy (ZIRP)  na mengineyo .

11.    ZACADIA imeshawasiliana na mashirika mbali mbali ambayop tayari yameonesha moyo wao wa kutaka kuisaidia Zanzibar na karibuni mwakilishi wetu huko Zanzibar atakutana na wawakilishi wa taasisi moja ya kimataifa ya Canada katika kutekeleza ushirikiano.

12.    Kuhusu Kadi ya Mzanzibari Mkaazi; Zacadia imewasiliana na idara inayohusika na ushirikiano wa Kimataifa huko Ikulu Zanzibar ili kulishughulikia suala hili kwa ajili ya wana Diaspora. Hata hivyo, suala hili limo kufanyiwa bill yake ili liingizwe katika Katiba kwani linahusiana na sheria na hivyo lazima kwanza lipitishwe na Baraza la Wawakilishi. Hata hivyo, kwa kusubiri vitambulisho hivyo, serikali ya Zanzibar kwa sasa inatoa vibali maaluum kwa wana Diaspora ili kuweza kurahisishiwa masuala yao huko Zanzibar kuanzia Uwanja wa ndege hadi katika masuala ya ukaazi na uendeshaji miradi yao binafsi.

13.    Zacadia imeshazungumza na SMZ  Kupata support katika mradi wowote wa kusaidia Zanzibar ili usimbuliwe kwa vifaa na michango utayopeleka Zanzibar.

14.    Kuwapeleka  vijana na watu wazima wa ki Zanzibari na nchi nyengine  kwenda kujitolea Zanzibar.

15.    Zacadia Hivi sasa tunaandaa  container(s) ya kupeleka Zanzibar itakayokuwa na vitu na vifaa mchanganyiko kwa miradi ya ZACADIA ya elimu, afya  kwa watoto mayatima na wa kawaida, wazee wasiojiweza na vijaana wasio na ajira. Kwa hili tumeahidiwa na shirika moja kubwa kusaidiwa kulipia ushuru wa container kwenda Zanzibar hadi kiwango cha Dola Elfu Sita.

16.     Kwa kutimiza hilo hapa juu Tumeiomba itupatie sehemu ya kuanzisha Zacadia Community Center in Zanzibar ili kuendesha program zetu mbali kupitia Ofisi zetu za  Managers  wetu wa  Unguja na Pemba. 

17.     Tuna Lengo kuanzisha Umbrella Organisation  ya kuunganisha Diaspora associations zote za Kizanzibari duniani  ZAIDI  (Zanzibar Alliance of International Diaspora Institutions)  kuwa na sauti, nguvu na umoja na kutafuta nyenzo/misaada  za kutekeleza malengo yetu kwa ufanisi zaidi  kwa pamoja.

18.    Kwa vile Diaspora organisation zinaweza  kuiingizia Serikali ya Zanzibar rasilmali  mbali mabli za missada yenye thamani kubwa na vifaa vya aina mbali mbali  kutoka nchi za nje  ikiwemo Canada kama vile nchi nyengine duniaini zinavyofaidika,  tunaishauri serikali ya Zanzibar ianzishe Zanzibar Diaspora Institute in Zanzibar ili itoe utaalamu na elimu  ya hali ya juu katika mambo na masuala  ya Diaspora  kwa  idara, wizara, watu, jumuiya za ndani na nje ya Zanzibar ili ziweze kufanikiwa kuleta utendaji na  tija kwa nchi yetu na watu wetu  na kupata misaada nchi za nje.

19.     Kwa vile Zacadia ni international organisation inayohusisha utaifa wa Zanzibar hapa Canada, Zacadia   imeweza kuwasaidia Wazanzibari katika masula na matatizo ya Immigration na ukaazi na kuthibitisha identity na sifa za Wazanzibari wenzetu kwa aajili ya maombi mbali mbali.

20.    BAADA YA MAELEZO MAFUPI   TUNAWAOMBA  NYOTE  BILA KUJALI JUMUIYA ULIYOTOKA KUJIUNGA NA SISI KUYATIMIZA MALENGO  HAYO  KWANI WITHOUT  YOU, YOUR FAMILY MEMBERS AND SOCIAL  NETWORKS  KUNA HATARI YA KUZIDIWA NA KAZI HII NZITO AMBAYO JAZA YAKE ITATOKA KWA ALLAAH SUBHANAHU WA TAALA.

Kuna mambo mengi mengine ya kuzungumza lakini wakati hauturuhusu, kwa hiyo mikutano ya aina hii itazidi kufanyika na ni matumaini yetu kwamba baada ya kusikia haya machache, itakuwa ni changamoto ya kuzidi kushiriki katika kuichangia ZACADIA ili iweze kufikia malengo haya. Timu yetu ni ya kujitolea na hakuna anayetarajia cho chote kutoka mfuko wa maendeleo wa ZACADIA, bali tunamtegemea Allaah kupata malipo kwa kuwasaidia ndugu zetu walioko katika shida huko Zanzibar.

Kwa haya machache, ZACADIA  INAWASHUKURU SANA  kwa kufika kwenu na kuweza kusaidia kuwachangia watoto wetu waliopoteza wazee wao kwa njia tafauti ikiwa ni pamoja na wale waliopotea kwa kuzama kwa meli iliyopoteza roho kadhaa na kuachwa mayatima kadhaa na vile vile kuwasAadia mamia ya ndugu zetu  wa kila umri wanaoteseka katika maisha yao ya  kila siku huko nyumbani Africa.

ZACADIA IS THINKING BIG…

Ahsanteni

Mungu awabariki nyote muliohudhuria na chi zenu pia kwa kutuunga mkono

Mungu ibariki Zanzibar na Watu wake

 Mungu Ibariki Canada –Amin

1 comment:

  1. Hongereni zcadia mmeonesha moyo huko tunako toka waznz, wingi waliyo pata bahati ya kukimbia haya mazila ya hapa znz wamejisahau, hawakumbuki kama kuna nduguzao na wa zee wao wako kwenye, mazila walotiwa na waafrika wenzao

    ReplyDelete

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.