Habari za Punde

Tukumbuke kufunga siku ya 'Aashuuraa. - tarehe 10 Muharram 1435


 

عَنْ ابْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ : مَا رَأَيْتُ النَّبِيَّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ يَتَحَرَّى صِيَامَ يَوْمٍ فَضَّلَهُ عَلَى غَيْرِهِ إِلّا هَذَا الْيَوْمَ يَوْمَ عَاشُورَاءَ وَهَذَا الشَّهْرَ يَعْنِي شَهْرَ رَمَضَانَ . " رواه البخاري 1867

Kutoka kwa Abdullah ibn ‘Abbaas, Allaah awawie radhi yeye na baba yake, amesema:

Sijapatapo kumuona Mtume Swalla Allaahu  ‘Alayhi Wasallam akiwa na hamu na shauku ya kufunga katika  siku aliyoifadhilisha kuliko siku nyengine isipokuwa siku ya ‘Aashuuraa na mwezi huu yaani mwezi wa Ramadhaan.  Bukhaari 1867

Mtume Swalla Allaahu ‘Alayhi Wasallam ametuhimiza waislamu kuifunga siku hii muhimu katika dini yetu kwani kufunga siku ya ‘Aashuraa ambayo ni tarehe 10 Muharram (Mfunguo nne) Allaah Subhaanahu Wata’ala hutusamehe madhambi yetu madogo madogo ya mwaka mzima uliopita.

Hii ni siku ambayo Allaah Subhaanahu Wata’ala alimuokoa NabiyuLlaahi Mussa ‘Alayhi Ssalaam, kutoka katika mikono ya Fir’aun aliyelaaniwa.

Ikiwa Mtume Swalla Allaahu ‘Alayhi Wasallam ameonesha hima na hamu ya kufunga katika siku hii je mimi na wewe?. Hivyo tuungane na Mtume wetu Swalla Allaahu ‘Alayhi Wasallam katika kuhakikisha tunaifunga siku hii ya ‘Aashuuraa kwani huko ndiko kufuata mafundisho na maagizo ya Ruwaza wetu , Swalla Allaahu ‘Alayhi Wasallam na kutekeleza Sunnah zake alizotuachia.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.