Habari za Punde

Ni Zanzibar au ni Unguja?


Ninapata taabu kuamini kwamba waandishi wengi  na wanataaluma ya habari wanashindwa kutumia matumizi sahihi ya visiwa vya Unguja, Pemba na Zanzibar.

Utaona wakati mwengine mwandishi anatumia jina la Zanzibar akimaanisha Unguja,wakati mwengine hutakiwa kutumika jina la Pemba lakini litatumika la Zanzibar. Ingawa kimaana huweza kuwa ni sawa lakini kimatumizi inawezekana kuwa na makosa

Tatizo hili nimeliona kwa waandishi wengi wa nyumbani, wa kigeni na kutoka upande wa pili wa Muungano wakijikuta wakiingia katika mtego huu.
Sehemu ambayo huwa nasikia kutajwa kama ni Unguja au Pemba ni pale panapotajwa mikoa ya Kusini/Kaskazini kama ni Unguja au Pemba na wilaya zake.

Mkanganyiko huu, kwa uoni wangu mdogo, umepelekea kwa kiasi kikubwa  kufa kidogo kidogo kwa jina la Unguja na badala yake kutumika Zanzibar kama ni Unguja  na ukiangalia kwa jicho pevu itapelekea uonevu tutakaowafanyia wana wa Kizanzibari ambao hujulikana hivyo kwa sababu ya kutoka katika Visiwa viwili vikuu vya Pemba na Unguja.

Tutafute njia muwafaka ya kutumika kwa majina haya mawili bila ya kuathiri jengine katika matumizi na mafhuum (maana) yake pia kabla ya kulipoteza jina la asili la Unguja kama hatujaanza sasa.

Na Mdau anaelienzi jina la Unguja

3 comments:

  1. Usilete utata na wewe Zanzibar inatumika kuainisha visiwa vya Unguja na Pemba pamoja na visiwa vidogo vidogo kama vile Tumbatu, Uzi, Kojani, Kisiwapanza na vinginevyo. Kwa maana ya nchi ya Zanzibar. Pia Zanzibar inaweza ikatumika kama ni mji wa Unguja.

    ReplyDelete
  2. hata kwa wenzetu pia hutumia Tanzania kama ni Tanganyika na ilhali Tanzania =Tanganyika+Zanzibar

    ReplyDelete
  3. mtoa mada napenda kukutoa hofu. Kwanza jua kuwa, kila chombo cha habari kina house style yake ya kuandishi hasa kwa namna hii kwa wandishi wao juu ya kuweka eneo kinapotoka chanzo cha habari ama alipo mwandishi?.

    Mfano: Karafuu yakamatwa Chakechake
    mwandishi ataandika: Na Sulumuni S. Sulumuni, Pemba.

    Mfano: Darajani machinga wagoma tena kufunga maduka
    mwandishi ataandika; Na Salma Hame Razu,Unguja

    au

    Umeme wakosekana kwa miaka 45
    Na Ali Swahiba Ahmed, Tumbatu
    kwa nini ameweka tumbatu? ameweka tumbatu kwa sababu ni eneo ambalo linatambulisha kwa moja kwa moja

    ama anaweka; Na Ali Swahiba Ahmed, Tumbatu,Unguja.

    ama anaweka;: Na Sulumuni S. Sulumuni, Chakechake, Pemba.

    kwaTanzania Bara; Na Andrew Chale, Bagamoyo ama Na Andrew Chale, Bagamoyo, Pwani
    au Na Andrew Chale, Pwani hii itakuwa tu endapo chanzo cha habari kimetoka ndani ya mkoa wa Pwani na hii ndio na sawa na kusema; Na Andrwe Chale, Unguja, lakini pia unaweza kusema Na Andrew Chale, Kizmkaz, Unguja.

    by Andrew Chale, mwandishi wa habari 0719076376.
    asante, usipagawe na uzuri wa picha ya kava, bali tazama filamu yenyewe..... na usiangalie by line by soma habari yenyewe.. ndani!

    ReplyDelete

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.