Na Joseph
Ngilisho,ARUSHA
WAKATI
wakaazi wa jiji la Arusha wakiwa bado na kumbukumbu ya kupoteza wapendwa wao
katika miripuko ya mabomu ya kurushwa kwa mkono katika kanisa la Katoliki
Olasiti na katika kampeni za uchaguzi, uwanja wa Soweto mwaka jana, watu 17
wamejeruhiwa vibaya na bomu la kutegwa wakati wakiangalia mpira katika baa ya
Arusha Night Park iliyopo Mianzini jijini Arusha.
Kati
ya majeruhi hao, 12 wamelazwa katika hospitali ya Mkoa Maunt Meru na mmoja
hospitali ya Selian, huku watano wakiruhusiwa, baada ya kupatiwa matibabu.
Aidha,
wagonjwa 11 walioko hospitali ya mkoa Mount Meru, mmoja hali yake ni mbaya, kutokana na kusagika
mfupa katika mguu wake wa kulia, hata hivyo uongozi wa hospitali hiyo unafanya
mawasiliano na Wizara ya Afya ili kujua kama
kuna uwezekano wa kuhamishiwa katika hospitali ya rufaa KCMC mkoani Kilimanjaro.
Akizungumza
kwenye wodi ya majeruhi hospitalini Mount Meru, Obeid Mbasha, alisema yeye
alikwenda kwenye baa hiyo kuangalia mpira , ila ilipofika majira ya saa 1:30 na
saa 2:00 usiku alisikia mripuko mkubwa
na kujikuta yupo chini huku wengine wakilia na kukimbia ovyo.
Kwa
upande wake mmoja wa majeruhi waliopatwa na mkasa huo, ambaye hakutaja jina
lake alisema alikuwa akiangalia mpira, ghafla alisikia kishindo kikubwa, kilichoambatana
na moshi hali ambao iliwashtua na kujikuta wakiwa wameumia.
Mmoja
wa wahudumu wa baa hiyo, Aneth Mushi, alisema yeye alikuwa amekwenda jikoni
kuchukua chakula ili awapelekee wateja wake waliomwagiza, wakati akibeba sahani,
ghafla alisikia kishindo na kelele za watu, hivyo alipoona hivyo alimwaga
chakula na kukimbia.
Mganga
Mkuu wa mkoa wa Arusha, Dk.Frida Mokiti, akizungumza baada ya kutembelea
majeruhi, alisema hospitali ya mkoa walipokea majeruhi 17 ambao kati yao mmoja alikwenda
Selian na watano waliruhusiwa baada ya kutibiwa.
"Lakini
hapa Mount Meru wamebaki watu kumi na
moja ambao kati yao wanaume nane na
wanawake watatu ila majeraha yao makubwa yapo miguuni na kwenye mapaja," alisema.
Alisema
hata hivyo mgonjwa mmoja ambaye hakumtaja jina lake, alisema hali yake siyo
nzuri, kwani ameumia sana na kusagika mfupa mdogo, hivyo wanafanya mawasiliano
na watu wa Wizara ya Afya wapate maelekezo ya kufanya au kama
kumuhamishia hospitali watajua.
Mganga
wa zamu katika hospitali ya Selian mkoani Arusha, Dk.Peter Mabula, alisema amepokea majeruhi mmoja na hali yake
inaendelea vizuri.
Hata
hivyo, Kamanda wa Polisi, Liberatus Sabas aliyekuwa eneo la tukio muda mwingi
na kikosi cha ukaguzi wa mabomu, alisema hawezi kuzungumza chochote.
Kwa
upande wa mkuu wa mkoa wa Arusha,Magesa Mulongo alisema kuwa mripuko huo ni wa
bomu linaloonekana kutengenezwa kienyeji na kwamba wanaendelea kushirikiana na
wataalamu wa mabomu kutoka jeshi la wananchi JWTZ.
Alisema
tukio hilo limetokea majira ya saa 2:00
usiku, wakati watu wakiwa wanaangalia mpira na ndipo wakasikia kishindo kikubwa
na kinachosadikiwa kuwa ni bomu la kutengenezwa kwa mujibu wa taarifa za awali.
Wahudumu watano waliojeruhiwa katika baa hiyo
wametambulika kuwa ni Suzani Jacob (31)mkazi wa Mianzini, Joyce Williamu (29) mkazi
wa Moshono, Loice John(29) mkazi wa Sanawari, Evance Charles (24) na Peter
James(25) mkazi wa Ilboru.
Akizungumza
bungeni jana, Waziri wa Mambo ya Ndani, Matius
Chikawe, alisema uchunguzi wa awali unaonesha bomu hilo limetengenezwa kienyeji.
Alisema
watu walioshuhudia walimuona mtu mmoja akiweka bomu hilo
na kuliripua na baadae akaenda kwenye baa ya jirani ya Washington na kutega bomu jengine lakini
halikuwahi kuripuka.
Alisema
wataalamu wa bomu wamepelekwa jijini humo kufanya uchunguzi na kuwabaini wanaohusika.
No comments:
Post a Comment