Habari za Punde

Mwanafunzi akutwa amekufa

Haji Nassor na Bakari Mussa, Pemba
MAMIA ya wananchi wa shehia za Wawi,Wara na wapita njia nyengine, jana wameshuhudia mwili wa marehemu
MOHAMMED Soud Makame (17), ambae ni mwanafunzi wa kidato cha pili katika skuli ya sekondari Vikunguni, amekutwa amekufa ndani ya nyumba iliyokuwa haijahamiwa katika mtaa wa  Wawi wilaya ya Chake Chake Pemba.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, taatifa za tukio hilo zilitolewa na mtoto mmoja ambae aliukuta mwili huo ndani ya nyumba hiyo, wakati yeye alipokuwa akifukuza kuku.

Walisema baada ya kuuta mwili huo, waliamua kutoa taarifa kwa vyombo husika ikiwa ni pamoja na polisi, hospitali, sheha wa shehia ya Wawi na baadhi yao kupiga simu kwa waandishi wa habari juu tukio hilo.

Walisema waalimkuta marehemu akiwa na kitambaa ambacho wakati wa uhai wake alikuwa akikivaa kichwani, ingawa kwa jana walikikuta kikiwa shingoni mwake, mithili ya mtu aliejitia kitanzi.


Sheha wa  shehia ya  Wawi, Rashid Issa Juma, alisema alipokea taarifa za tukio hilo jana majira ya 5:40 mchana, baada baadhi ya wananchi kuushuhudia mwili huo wa marehemu na ndipo alipotoa taarifa kituo cha polisi wilaya ya Chake Chake, ambapo baadae walifika kwa shughuli zao za kisheria.

Baba mzazi wa marehemu huyo, Soud Makame, alisema mwanawe amekuwa na kawaida kila siku kulala ndani lakini siku ya tukio hakulala, ingawa hakuwa na wasiwasi wowote kwa vile anaweza kulala hata kwa rafiki wake.

“Kawaida yake hasa ni kulala nyumbani mwangu, ila juzi ndio hakuja lakini hata mimi sikuwa na wasisi na leo (jana) nimepokea taarifa ya mshituko kwamba amekutwa amefariki,” alisema.

Daktari Ali Hamran Mohamed wa hospitali ya Chake Chake, alieufanyia uchunguuzi mwili wa marehemu,alisema inaonesha kifo chake kilisababishwa na kuekewa kitu kizito shingoni.

“Inaonekana marehemu ama amewekewa kitu kizito shingoni mwake, maana kabla ya kupoteza uhai ulimi wake umetoka nje, na hasa kwa vile amekutikana na michubuko shingoni,” alisema.


Hili ni tukio la nne kwa mwaka huu mkoa wa kusini Pemba kwa wananchi kuokota miili ya watu waliofariki.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.