Habari za Punde

Kampuni ya Perdue kuwakomboa wafugaji kuku

Na Khamis Amani
KAMPUNI ya uuzaji wa kuku ya PERDUE iliopo nchini, imo mbioni kukamilisha kiwanda cha uboreshaji kuku wa viungo na kuuzwa nje ya nchi.

Mara baada ya kiwanda hicho kukamilika kitawanufaisha baadhi ya wafugaji wa kuku kwa kuwa na soko la uhakika la kuuzia kuku wao.

Kampuni hiyo inayouza kuku kutoka nje ya nchi kwa takriban miaka miwili sasa, imesema hali hiyo itainua kipato cha wafugaji na kuwakwamua katika hali ngumu ya umasikini inayowakabili.

Hayo yalielezwa na Meneja Operesheni wa kampuni hiyo, Christopher Kontonasios, wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi.

Alisema, kiwanda hicho ambacho kazi yake kubwa itakuwa ni kuboresha kuku waliotiwa viungo vinavyopatikana Zanzibar na kuuzwa ndani na nje ya nchi huku wakiwa na utambulisho wa kutengenezwa Zanzibar.


Alisema kuwepo kwa kiwanda hicho kutapanua ajira kwa vijana, kuwanufaisha wafugaji wa kuku kwa kukunua kuku wao baada ya kuidhinishwa ubora wao na bodi ya kampuni hiyo, pamoja na kuitangaza Zanzibar katika soko la Afrika Mashariki na soko la kimataifa.

Alisema jengo hilo liliopo Maruhubi linakaribia kukamilik, na wakati wowote kuanzia sasa vifaa vya awali vitakavyotumika katika kiwanda hicho vitawasili.

Aliiomba serikali kuwa karibu na wawekezaji na kuwapatia ufumbuzi wa haraka pale wanapotaka huduma kwa ajili ya vitega uchumi vyao, ili viweze kukamilika katika wakati uliopangwa.

Kuhusu bidhaa ya kuku hao, wanaouzwa hapa nchini, 

Meneja huyo alisema kuku hao ni halali na salama kwa mlaji na ni moja ya kuku bora duniani ambao wamepatiwa vyeti kadhaa vya kimataifa kwa ubora wake.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.