Na
Mwandishi Wetu.
BAADHI
ya wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba, wameupiga marufuku Umoja wa Katiba ya
Wananchi (UKAWA), kutokwenda kufanya mikutano katika majimbo yao,ili kuiepusha
nchi kuingia kwenye ghasia.
Wajumbe
hao, waliyasema hayo jana wakati wakichangia sehemu ya kwanza na ya sita ya
rasimu ya katiba mjini Dodoma .
Mwakilishi
kutoka makundi ya dini, Nouman Juma Jongo, akitoa maoni yake, alisema
analishangaa kundi la UKAWA kuamua kuitumia Zanzibar kuendesha maandamano na kuiingiza
nchi kwenye vurugu.
Alisema
lazima kundi hilo litambue kuwa Zanzibar
imechoka na vurugu za aina yoyote na haikubaliki kuona viongozi kwa UKAWA
kutangaza kuiutumia Zanzibar kama
ndio nchi ya kuendesha harakati zao.
Alisema
wananchi wa Zanzibar
hivi sasa wapo katika kuendeleza umoja wa kitaifa baada ya kuchoshwa na vurugu zilizosababisha
vifo vya watu.
“Zanzibar
tumechoka na vurugu tuangalie yaliotokea miaka ya nyuma, watu walikufa na sasa
Zanzibar iko vizuri, kwa nini kambi ije ifungwe huku wakati hapa watu
wameridhiana, hatutaki kwani wanaoathirika ni Wazanzibari,” alisema.
Kwa
upande wake, Dk. Maua Abeid Daftari alilitaka kundi hilo lifanye mikutano yake
Tabora au Singida ili nao wao waone raha, lakini Mwenyekiti wa bunge hilo,
Samuel Sitta, alisema hata watu wa Tabora hawawataki UKAWA kwa sababu hawapendi
vurugu.
Alisema
ni vyema viongozi hao wakaona umuhimu wa kukaa pamoja, kwani ajenda waliyopanga
kuitumia kwenye maandamano yao ikiwemo udini, ukabila na siasa chafu,
vitachangia kuvuruga amani.
“Mimi
naona hapa kuna jambo kwanini vurugu hizi ziletwe Zanzibar na viongozi wake
kama Lipumba, alipaswa kupeleka UKAWA mji wa Tabora, Lisu nae aende nao huko
Singida, tumechoka na vurugu Zanzibar,” alisema.
Nae
Tawhida Galos Nyimbo, alisema vijana wa Zanzibar
hawatakuwa tayari kuona kundi la UKAWA linaruhusiwa kufanya mikutano yake kwani
wamechoka kuifanya Zanzibar
chambo cha vurugu.
“Vijanaa
wamenituma wanasema hawautaki UKAWA, sasa watafute pa kwenda kwani wana uwezo
wa kwenda mikoa mingine na sio Zanzibar pekee,” alisema.
Waziri
wa Mawasiliano na Uchukuzi, Dk. Harison Mwakyembe,akitoa mchango wake
aliwaripua wanasheria wa UKAWA, akiwaita ni wanasheria wanaostahili
kunyanganywa vyeti vyao kwa vile wamekuwa wakisema uongo.
Alisema
viongozi hao wameamua kutumia taaluma yao
kinyume na malengo ili kuipotosha jamii na kutimiza matakwa yao .
Alisema
inashangaza kuona wanaojiita wasomi wa sheria, kudai Zanzibar inaweza kuwa
Hongkong, wakati kuna visiwa vingi duniani havijafanana na nchi hiyo.
Mapema akitoa maelezo yake, Mwenyekiti wa Bunge
hilo,Samuel Sitta, alisema kikao kinachoendelea hakihitaji akidi kwani kwa njia
moja ama nyengine katiba mpya itapatikana
ndugu jongo wewe huwezi kuwa msemaji wa wazanzibari, tumechagua mwl sefu kuwa msemaji na mtetezi wetu , na yeye akitereza kukubaliana na watanganyika tutamtimua tutafute mwengine mwenye kuweza kutukombolea visiwa vyetu
ReplyDeleteUkweli huyu jongoo anatoka Zanzibar au, mbona kiherehere hivi na akapime akili yake kwanza
ReplyDelete