Shemsia
Khamis na Habiba Zaral, PEMBA
MKUU
wa Mkoa wa Kusini Pemba, Juma Kassim Tindwa, amewataka wananchi kisiwani humo,
kuwa wamoja katika kuudumisha muumgano wa Tanganyika
na Zanzibar kwa
maslahi ya sasa na baadae.
Alisema
maazimio ya Muungano ni kuwakusanya Waafrika katika kupata haki zao, ikiwemo
kuwawekea makaazi mazuri na kuondoa ubaguzi, kwa lengo la kuleta maendeleo.
Aliyasema
hayo Chake Chake, alipokuwa akizungumza
na wananchi katika maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar .
Alisema
usharikiano na maelewano yaliyoanzishwa na waasisi wa Muungano, yakiendelea
kudumishwa nchi inaweza kuwa salama, sambamba na kukuza umoja uliopo.
Alisema
kazi ya serikali ni kuhakikisha nchi inakuwa na amani na utulivu kwa njia
yoyote, ili wananchi waweze kuishi kwa salama, ambapo Muungano umeweza kusaidia
katika hilo .
Akizungumzia
mchakato wa katiba unaoendelea, alisema muundo wa serikai uliopo unakidhi
mahitaji ya wananchi.
Kwa
upande wake, Ofisa tawala mkoa wa kusini Pemba, Hanuna Ibrahim Massoud,
alisema Muungano umewafanya wananchi
wote kuwa wamoja, hivyo ni vyema kuuenziwa ili uweze kudumu.
Nae
Ofisa Mipango mkoa wa kusini Pemba, Matar Zahor Massoud, akisoma risala kwa
niaba ya mkoa alisema, ni vyema wananchi kuunga mkono Muungano uliopo kwa faida
ya wote.
Maadhimisho
siku ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, huadhimishwa ifikapo Aprili 26 kila
mwaka, ambapo kauli mbiu ya mwaka huu inasema, utanzania wetu ni muungano wetu,
tuulinde, tuimarishe na kuudumisha.
No comments:
Post a Comment