Na Jumbe
Ismailly, IKUNGI
WAKAZI
28 wa kata nne zilizopo tarafa aya Ikungi, mkoani Singida wamejeruhiwa vibaya
baada ya kung’atwa na mbwa wanaodhaniwa kuwa na kichaa.
Kata
zilizoathirika na tukio hilo lililotokea Februari 22 na Aprili 22, mwaka huu ni
pamoja na Mang’onyi, Unyahati, Ikungi, Isuna kijiji cha Mpetu.
Ofisa
afya wa kata ya Ikungi, Agnesi Lucas John, alisema kati ya watu walioumwa na
mbwa hao na kufikishwa kituo cha afya cha tarafa ya Ikungi,k 10 ni kutoka kata
ya Mang’onyi, Unyahati watu sita,Ikungi watu watano, Dung’unyi mtu mmoja, Isuna mmoja na Mpetu mmoja.
Alitoa
wito kwa watu wanaofuga mbwa wawapeleke mbwa wao kupatiwa chanjo zinazotolewa
na maofisa mifugo kwenye maeneo yao .
Aidha,
aliagiza mbwa wanaofugwa wafungwe wakati wa mchana ili wasizurure ovyo kwani
endapo wazurura wanaweza kukutana na mbwa mwenye kichaa na kushambuliwa na
hatimaye nao kupata kichaa.
No comments:
Post a Comment