Habari za Punde

Achinjwa kama kuku akituhumiwa kuiba ng’ombe

Na Mwandishi wetu
MTU mmoja ameuawa kwa kuchinjwa shingoni na kukatwa mguu baada ya kutuhumiwa kuiba ng’ombe.
Tukio hilo limetokea katika kijiji cha Tunduni wilaya ya kati Unguja.
Kwa mujibu wa taarifa ya polisi, marehemu alikutwa na mauaji hayo baada ya kutuhumiwa kuiba ng’ombe mwishoni mwa wiki iliyopita.
Marehemu alivamiwa na watu wenye hasira usiku akijiandaa kupakia nyama kwenye gari lake ambayo inaaminika ilitokana na ng’ombe wa wizi.

Baadhi ya mashuhuda walisema, watuhumiwa wengine wa tukio hilo walipigwa na kujeruhiwa vibaya.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.