Habari za Punde

Shamba la Balali lataifishwa

Na Judith Mpalanzi, Kilombero
SHAMBA lililokuwa likimilikiwa na aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu Tanzania (BoT) hayati Daudi Balali, ni miongoni mwa mashamba yaliyofutiwa umiliki na kukaribisha wawekezaji wapya.

Hayo yamo kwenye taarifa ya Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kilombero, Daudi Ligazio.

Alisema tayari mchakato wa kufutwa na kubadilishwa matumizi mashamba hayo zipo katika hatua za kati.

Alisema kwa mujibu wa kumbukumbu za halamashauri, wawekezaji wengi hawapo wilayani na wengine nchini badala yake wamekuwa wakiyatumia maeneo hayo kama nguzo ya uchumi wao.

“Uamuzi wa kukufikia hapa ni baada ya halmashauri kubaini kuwa mashamba mengi makubwa yaliyomilikishwa wawekezaji wilayani humo ni chanzo kikuu cha cha migogoro ya ardhi kutokana na kutelekezwa na kubaki mapori," alisema.


Alisema tayari watendaji na wenyeviti wa vijiji wilayani humo wameagizwa kuainisha mashamba hayo ili zoezi likamilike kwa wakati.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.