Habari za Punde

Mahujaji watakiwa kuwa wamoja.

Na Mwanajuma Mmanga
 
WAISLAMU wanaokwenda kutekeleza ibada ya hijja, wametakiwa kuwa na umoja na mshikamano ili kufanikisha ibada hiyo.
 
Kadhi Mkuu wa Zanzibar, Sheikh Khamis Haji Khamis, alisema hayo wakati akifunga semina kwa Mahujaji hao Msikiti Muwashawr Mwembeshauri.

Aidha aliwataka kutekeleza masharti ya ibada hiyo ambayo inamuwajibikia kila Muislamu alie na uwezo.

Aliwataka viongozi wanaofuatana na mahujaji kutekeleza wajibu wao ili mahujaji hao watekeleze ibada kwa utulivu.

Kwa upande wa mahujaji, aliwahimiza kuzingatia maagizo ya viongozi wao ikiwemo kuepuka kutembea pekee yao.

Sheikh Khamis aliwataka wahudumu wa afya kuwasaidia mahujaji watakaopata matatizo wakati wakitekeleza ibada hiyo.


Nae Katibu Mtendaji wa Umoja wa Taasisi ya Hijja Zanzibar, (UTAHIZA), Ali Khatib Mranzi, alisema idadi ya mahujaji wa Zanzibar inaongezeka kila mwaka.

Alisema lengo ni kupeleka mahujaji 1,900 katika hijja ya mwaka ujao.


Hata hivyo, aliwataka Waislamu wengine wenye uwezo kutekeleza ibada hiyo ambayo ni miongoni mwa nguzo tano za Uislamu.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.