Habari za Punde

Sitta: Baadhi ya nyaraka zinasomwa makanisani hazina utukufu wa Mungu

Na Mwandishi wetu, Dodoma
MWENYEKITI wa Bunge Maalum la Katiba, Samuel Sitta, amesema baadhi ya nyaraka zinazosomwa makanisani ni upuuzi mtupu na hazina utukufu wa Mwenyezi Mungu.

Akiwakaribisha wageni waliofika bungeni jana, ambao ni waumini wa dini ya kikiristu, Sitta, aliwataka wageni hao kuwa waangalifu na baadhi ya nyaraka zinazosomwa makanisani kwa sababu ni za kipuuzi na hazina utukufu wa Mungu.

Hivi karibuni Jumuiya ya Kikiristo Tanzania (CCT) ilitoa waraka uliokuwa ukisomwa makanisani kupinga Bunge Maalum la Katiba.


Akitoa idadi ya wajumbe wa bunge hilo, Sitta, alisema idadi ya Wabunge wote wa Bunge Maalum ni 629, kati ya hao idadi ya wabunge wa Tanzania Bara ni 419 na Zanzibar ni 210.


 Aliseka akidi inayotakiwa kupitisha rasimu ya katiba ni 280 kwa Tanzania Bara na 140 kwa Zanzibar.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.