Na Haji Nassor, Pemba
Vijana kisiwani Pemba,
wametakiwa kujiepusha na makundi ya watu wanaopita na kuwakusanya wakidai
wanajadili rasimu ya pili ya katiba.
Kuali hiyo imetolewa na Naibu
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM
Zanzzibar (UVCCM), Shaka Hamdu Shaka, wakati akizunguma na vijana wa chama
hicho kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika uwanja wa Gombani kongwe.
Alisema baadhi ya wajumbe wa
bunge la katiba, wamekuwa wakipita
mitaani na kuwakusanya wananchi na kuichambua katiba hiyo,ambapo maoni yao
hayapelekwi popote.
Alisema kwa vile vijana ndio
nguzo ya kutegemea katika taifa, ni vyema wasighilibiwe kwa njia yoyote ile.
Alisema kwa sasa kazi ya
kuichambua katiba hiyo inakwenda vyema na hakuna matusi tena kama ilivyokuwa
awali.
Aliwahimiza vijana wa CCM
kisiwani Pemba, kujipanga vyema na uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 ili kuhakikisha
CCM inanyakua majimbo kisiwani humo.
Aidha alisema katika
kufanikisha hilo umoja, mshikamano na utayari wa kila kiongozi na mwanachama
unahitajika kwa nguvua zote.
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa kusni
Pemba, Abdalla Hamad Mshindo, aliwataka wanachama wa UVCCM kutembelea kifua
mbele bila ya woga na kueleza ukweli juu ya kazi za CCM zinavyofanywa.
Katika risala yao, vijana wa mikoa
miwili ya Pemba, walisema hatua ya Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shien,
kuendelea kuisimamia vyema ilani ya CCM ni jambo la kuungwa mkono.
No comments:
Post a Comment