Na Kauthar Abdalla
Waziri wa Habari, Utamaduni,
Utalii na Michezo, Mhe. Said Ali Mbarouk, ameasa kwamba mitizamo ya kisiasa na kiitikadi isipewe
nafasi katika uendeshaji wa shughuli za jumuiya.
Alisema uzoefu unaonesha
shughuli za kisiasa zikitawala, msukumo
wa maendeleo huvia na ndio chanzo cha kusambaratika kwa jumuiya nyingi.
Alieleza hayo katika uzinduzi
wa Jumuiya ya Maendeleo ya Watu wa Junguni (JUMJU) uliofanyika hoteli ya
Bwawani.
Alisema jumuiya zenye kusukuma
maendeleo zina faida kwa jamii na serikali na ndio kichochoe cha kuleta
maendeleo.
Alisema kuna jumuiya nyingi zilizoanzishwa lakini zimeshindwa kufikia
malengo kutokana na wanajumuiya kutokwa na umoja wakati wa utekelezaji.
Alisema anaamini jumuiya hiyo
itaongeza kasi ya maendeleo katika kijiji hichi kilichomo ndani ya jimbo la
Gando.
Katibu wa jumuiya hiyo, Sada
Khamis Juma, alisema lengo la kuundwa jumuiya hiyo ni kuunganisha nguvu za watu
wa kijiji cha Junguni walioko nje ya kijiji hicho ili kutatua changamoto
zinazowakabili watoto na ndugu zao.
Alisema moja ya changamoto
inayowakabili wakazi wa kijiji hicho ni ni kutokuwepo walimu wa kutosha,
maabara, maktaba na kompyuta.
No comments:
Post a Comment