Habari za Punde

ZSTC yasaidia wajasiriamali Pemba

Na Marzouk Khamis, Maelezo-Pemba
MKURUGENZI Fedha wa Shirika la Biashara la Zanzibar (ZSTC), Ismai Omar Bai, amesema Shirika limepata mafanikio katika ununuzi na uimarishaji wa zao la karafuu kutokana na ushirikiano inaoupata kuttoka kwa wakulima na wadau wa zao hilo.

Alisema shirika litaendelea kugawa faida inayopatikana kutokana na zao hilo kwa kusaidia maendeleo ya jamii kila hali inaporuhusu.
Aliyasema hayo kwa niaba ya Mkurugenzi Mwendeshaji wa Shirika hilo,Chake Chake katika hafla maalum ya kukabidhi mashamiana kwa wajasiriamali wa soko la Jumapili (Sunday Market) ambayo yametolewa na shirika hilo.
Alisema ZSTC sasa imeelekeza nguvu zake kuisadi jamii katika shughuli za maendeleo ikiwemo vikundi vya ushirika vya wajasiriamali na wakulima wa zao la kafaruu kwa lengo la kuinua uchumi wao.

Alisema miongoni mwa misaada inayotolewa na shirika hilo inaelekwezwa katika miradi ya ujenzi wa barabara za vijijini ikiwemo ya Ngo'mbeni Mkoani na Kiwani, miradi ya ujenzi wa skuli , biashara, umeme kwa vituo vya ununuzi wa karafuu na vikundi vya ujasiriamali.
Mapema akikabidhi mashamiana hayo kwa wajasiriamali hao, Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba, Mwanajuma Majid Abdalla, aliwasisitiza kuyatumia vizuri na kulitumia soko hilo kuendelea kibiashara.
Katiak hafla hiyo Mkuu wa Mkoa alikabidhi mashamiana mawili yenye thamani ya shiling milion14.1.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.