Habari za Punde

ZATI Yaandaa Chakula cha Usiku kwa Wanachama Wake na Wageni wao

Mwenyekiti mstaafu wa ZATINdg.Simai Mohamed Said akizungumza wakati wa hafla ya chakula cha usiku kilichoandaliwa na ZATI kuwapongeza na kutathimini mafanikio ya jumuiya hiyo kwa michango ya wawekezaji Zanzibar.katika sekta ya Utalii iliofanyika katika ukumbi wa hoteli ya Zanzibar Beach resort mazizini Zanzibar
Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania Balozi Egon Kochanke, akizungumza katika hafla ya chakula cha usiku kilichoandaliwa na Jumuiya ya ZATI Zanzibar iliofanyika katika ukumbi wa hoteli ya Zanzibar Beach Resort mazizini Zanzibar.
Mgeni Rasmin Balozi wa Ujerumani Tanzania Balozi.Egon Kochanke, akimkabidhi Cheti Kamishna wa Polisi Zanzibar,Ndg Hamdan Omar Makame, kwa Mchango wa Jeshi la Polisi katika kulinda Usalama wa Watalii na Raia kwa ujumla, wakati wa hafla ya chakula cha usiku kilichoandaliwa na jumuiya ya ZATI Zanzibar katika ukumbi wa hoteli ya Zanzibar Beach Resort Mazizini Zanzibar.
Mgeni Rasmin Balozi wa Ujerumani Nchini Tanzania Balozi.Egon Kochanke, akimkabidhi Cheti Mkurugenzi wa Vitega uchumi Zanzibar ZIPA,Ndg.Salumu Nassor., wakati wa hafla ya chakula cha usiku kilichofanyika Zanzibar Beach Resort mazizini.Ikiwa ni kuthamini Mchango wa ZIPA kwa Mchangao wao kwa Wawekezaji walioekeza Zanzibar na Wawekezaji Wazawa.wa Zanzibar.
 Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania, Egon Kochanke akiwa na Mwenyekiti wa ZATI, Abdulsamad Said baada ya Balozi huyo kuwasili kwenye hafla hiyo jana.
                     Balozi Kochanke akishiriki kununua tiketi za Tambola kwenye hafla hiyo jana.






        Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania kishiriki hafla ya chakula cha usiku kilichoandaliwa na ZATI kwa                           wanachama wake na wageni wengine kwenye hoteli ya Zanzibar Beach Resort jana
(Picha na Martin Kabemba) .

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.