HALI ya utupaji taka taka ovyo pembezoni mwa mwa bahari kwenye kisiwa cha Kojani wilaya ya wete Pemba, umeonekana kupungua kwa kiwango kikubwa, baada ya wananchi wake kupata taaluma ya usafi wa mazingira kupitia jumuia ya vijana jimbo la Kojani KOYMOCC, (Picha na Haji Nassor, Pemba
MITARO
ya maji machafu imetajwa kuwa ni miongoni mwa changamoto kubwa, ambayo
huchangia kuchafua mazingira ya Kisiwa cha Kojani Pemba, ambapo hayo
yalishuhudiwa wakati wananchi kisiwani humo walipokuwa na ziara ya kuangalia
hali ya usafi wa mazingira, chini ya Jumuia ya Vijana jimbo la Kojani KOYMOCC,
(picha na Haji Nassor, Pemba).
No comments:
Post a Comment