Habari za Punde

Dua maalum ya kitaifa kuiombea nchi yetu ya Zanzibar

Uongozi wa Jumuiya ya Baraza la Maulid Tomondo Zanzibar (blmt), ukishirikiana na ofisi ya Mufti Zanzibar pamoja na Taasisi za Kiislamu, unawatangazia na kuwaomba waislamu na wananchi wote kwa ujumla kuhimizana kuhudhuria katika shughuli ya dua maalum ya kitaifa ya kuiombea nchi yetu itakayojumuisha Maulid ya bwana Mtume Muhammad (S.A.W), itakayofanyika siku ya Jumamosi ya tarehe 21 Machi 2015 kuanzia saa moja  (1) usiku hadi saa tano (5) usiku katika uwanja wa Amaan Stadium mjini Zanzibar.

Sala za Magharibi na Isha zitasaliwa kwa nyakati zake na kwa jamaa kubwa hapo hapo uwanjani.

Shughuli hii ambayo ni kwa ajili ya wanaume tu itahudhuriwa na wanazuoni mbali mbali kutoka ndani na nje ya nchi yetu, waheshimiwa viongozi wetu wa kiserikali, asasi za kiraia, wafanyabiashara n.k. 

Vyombo vya ulinzi na usalama vitakuwepo kusimamia amani na utulivu wa shughuli hio mwanzo hadi mwisho.

Milango ya viwanja vya Amaan itakuwa wazi kuanzia saa kumi na mbili (12 ) za jioni

Waumini nyote mnakaribishwa, shime shime shime tuhudhurieni kwa wingi  sana tukamuombe  Mwenyezi Mungu amani kwa ajili ya visiwa vyetu.


Usafiri wa mashamba ng'ambo na mijini utakuwepo in shaa Allaah

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.