Habari za Punde

Hitma ya Marehemu Salmin Awadh leo

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akijumuika na Viongozi na waislamu katika kisomo cha Hitma ya Marehemu Salmin Awadh aliyekuwa Mwakilishiwa Jimbo la Magomeni (CCM) iliyosomwa leo jioni katika Msikiti wa Mushawal Mwembeshauri Mjini Unguja hitma hiyo ilihudhuriwa na Waumini na Wanachama wa Chama cha Mapinduzi,[Picha na Ikulu.]

Baadhi ya Waislamu na Viongozi mbali mbali na wananchi wakiwa katika kisomo cha Hitma ya kumuombea Dua Marehemu Salmin Awadh aliyekuwa Mwakilishi wa Jimbo la Magomeni (CCM) Mjini Unguja aliyefariki hivi karibuni Hitma hiyo ilisomwa leo jioni katika Msikiti wa Mushawar Mwembeshauri,[Picha na Ikulu.]

Katibu wa Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Fadhil Soraga akitoa mawaidha baada ya kisomo cha Hitma ya Marehemu Salmin Awadh aliyekuwa Mwakilichi wa Jimbo la Magomeni (CCM) Mjini Unguja aliyefariki hivi karibuni Hitma hiyo ilisomwa leo jioni katika Msikiti wa Mushawal Mwembeshauri,[Picha na Ikulu.]

Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai akitoa shukurani kwa Viongozi mbali mbali Waislamu na Wananchi na wapenzi wa CCM baada ya kisomo cha Hitma Marehemu Salmin Awadh aliyekuwa Mwakilichi wa Jimbo la Magomeni (CCM) Mjini Unguja iliyosomwa leo katika Msikiti wa Mushawal Mwembesahauri Marehemu alifariki hivi karibuni na kuzikwa Makunduchi Mkoa wa Kusini Unguja,[Picha na Ikulu.] ]

STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
       Zanzibar                                                                                               1.3.2015
---
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Ali Mohamed Shein  leo ameungana na viongozi mbali mbali wa dini, vyama na serikali pamoja na wananchi kutoka maeneo mbali mbali ya Zanzibar katika hitma ya kumuombea marehemu Salmin Awadh Salmin aliyekuwa Mwakilishi wa Jimbo la Magomeni

Hitma hiyo iliyotayarishwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM )Zanzibar, ilisomwa katika Masjid Mushawar, Mwembeshauri mjini Zanzibar na kutanguliwa na  Qur-an Tukufu iliyosomwa na Sheikh Sharif Abdulrahman.

Viongozi wa dini nao walipata fursa ya kutoa mawaidha kwa mnasaba wa tukio hilo ambapo Katibu Mkuu wa Mufti Sheikh Fadhil Soraga alitoa mawaidha juu ya mada inayohusu mauti pamoja na haja ya kumuombea dua maiti.

Aidha, Sheikh Soraga alitumia fursa hiyo kutoa visa mbali mbali vya Masahaba juu ya mauti kikiwemo kisa cha mauti yaliyomfika Bwana Mtume Mohammad (S.A.W).


Nae Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Vuai Ali Vuai alitoa shukurani kwa viongozi wa dini, vyama vya siasa na Serikali pamoja na wananchi waliohudhuria katika Hitma hiyo.

Naibu Vuai alisema kuwa Marehemu Salmin Awadh mauti yamemchukua akiwa katika shughuli za kuimarisha Chama Cha Mapinduzi huko Kisiwandui mjini Zanzibar, Sambamba na hayo, Naibu Vuai alitumia fursa hiyo kutoa shukurani kwa Alhaj Dk. Shein kwa faraja zake kwa viongozi alizozitoa juu ya msiba huo.

Miongoni mwa viongozi waliohudhuria ni Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khamis Haji, Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai, Mawaziri, Wabunge,Wawakilishi na viongozi wengine wa Serikali, dini na vyama vya siasa pamoja na wananchi kutoka Mikoa ya Unguja Kichama na Kiserikali.

Rajab Mkasaba, Ikulu
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822  


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.