Na Himid Choko, BLW
Mratibu
wa Programu ya Jinsia , Wizara ya Uwezeshaji , Ustawi wa Jamii, Vijana
Maendeleo ya Wanawake na Watoto ndugu
Halima Abdulrahman amewahimiza Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kutumia ushawishi wao kwa nguvu zote, ili
kuhakikikisha kwamba bajeti ya serikali na zile za kisekta zinazingatia
mahitaji ya makundi mbali mbali
katika jamii .
Ndugu
Halima ametowa wito huo leo wakati akiwasilisha mada inayohusu Bajeti na Mtazamo wa Kijinsia katika semina ya
Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi huko Z- Ocean Hotel Chuwini.
Amesema kwa kuwa
Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi
ndio waidhinishaji wa ukusanyaji wa
mapato na matumizi ya serikali, hivyo
wana wajibu wa kuhakikisha
kwamba serikali inapanga bajeti kwa mtazamo wa kuzingatia
makundi mbali mbali ikiwemo kijinsia ni
zana inayotusaidia kutekeleza misingi ya utawala bora ambayo ni usawa ,
uwajibikaji na ufanisi.
Aidha
ndugu Halima amesema Wawakilishi wanapaswa kuhakikisha kwamba bajeti za serikali pia zinazingatia uwepo wa
vifungu vitakavyochangia kukuza uwiano na usawa wa kijinsia katika kupata
huduma mbali mbali ikiwemo kuwawezesha wanawake
kushiriki kikamilifu katika kuleta maendeleo ya nchi.
Halima
amevitaja Baadhi ya Vifungu ambavyo vinafaa kuzingatiwa katika bajeti kuwa ni
pamoja Vifungu vinavyolenga kukuza ajira
kwa wanawake, kukuza upatikanaji wa mikopo na taaluma ya ujasiriamali kwa
wanawake na Vifungu vinavyolenga
kutekeleza programu za elimu na Afya kwa wanawake.
Aidha
ndugu Halima ametaja vifungu vyengine vinavyofaa kuzingatiwa katika bajeti kuwa
ni Vifungu kwa ajili ya huduma za hifadhi ya jamii katika
kustaafu, kukosa ajira, ugonjwa, uzee na kukosa uwezo wa kufanya kazi pamoja na vile vinavyolenga kusaidia kukuza ufanisi katika shughuli za
kilimo na kuboresha huduma ya maji mijini na vijijini
Nae
Mkuu wa kitengo cha idadi ya watu Tume ya Mipango Salama Ramadhan Makame akiwasilisha mada inayohusu Idadi ya Watu na Maendeleo ya Kiuchumi na
Kijamii amesema hivi sasa kunachangamoto
kubwa ya ongezeko la ukuwaji wa idadi ya
watu linalochangiwa na uzazi, vifo na
uhamiaji hivyo uchambuzi wa kina na
mahitaji ya kisera yanahitajika ili kuoanisha
masuala ya idadi ya watu na maendeleo.
Amesema
hatua hiyo itasaidia ongezeko la idadi ya watu isiwe kikwazo bali iwe fursa katika uzalishaji mali na maendeleo.
Amesema kutokana na athari nyingi zinazotokana na
kasi ya ongezeko la idadi ya watu katika
ardhi na kimazingira ipo haja ya kuaandaa mipango madhubuti ya maendeleo ya
utekelezaji halisi wa mipango miji, ujenzi wa nyumba za ghorofa, matumizi ya
nishati mbadala na uzazi wa mpango.
Semina
hiyo ya siku nne ilikua ni maalum kwa wajumbe wa Baraza la Wawakilishi ambao wanatarajiwa kuaza kuijadili Bajeti ya
serikali kuazia kesho (leo Jumatatu)
kuwajengea uwezo ili waweze kuijadili vyema bajeti.
Akifunga semina hiyo Makamu wa Pili wa Rais wa
Zanzibar Balozi seif Ali Idd amesema kutokana na taaluma iliyopatikana katika semina hiyo anatarajia kupata michango
mizuri na yakujenga
kutoka kwa wajumbe wajumbe wakati
wa mjadala wa bajeti hapo kesho.
Amesema
ukuaji na uimarikaji wa uchumi wa taifa unategemea matokeo ya uchaguzi Mkuu
ujao ambao anategemea utakuwa wa amani na utulivu.
Amesema serikali
itahakikisha kwamba tume ya uchaguzi inaendesha uchaguzi wa haki , uhuru
na uwazi.
Amesema
uchaguzi uliosalama utapelekea kwa wageni, watalii na wawekezaji kuvutika kuja
kwa wingi hatimae kukuza pato la taifa
litakalosaidia kuiimarisha uchumi wa taifa.
Aidha
amesisitiza suala la umuhimu wa kutunza mazingira na uwazi katika bajeti .
No comments:
Post a Comment