Habari za Punde

Kilele cha siku ya wafanyakazi Duniani May Day Pemba

WALIOACHA madawa ya kuleavya wakiwa wanalelewa kwenye nyumba za kurekebisha tabia Sober House, wakiwa ni miongoni mwa makundi yalioshiriki maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani, ambapo kwa kitaifa kwa Zanzibar, zilifanyika Chake chake Pemba, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi dk Ali Mohamed Shein akiwapungia mkono wafanyakazi walijitokeza kwenye maandamano yaliopamba kilele cha maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani yaliofanyika Kisiwani Pemba kitaifa kwa Zanzibar, (Picha na Haji Nassor, Pemba)..
 WANFAYAKAZI wa kapuni ya simu ya T.T.C.L wakipita mbele ya mbele ya mgeni rasmi rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani, ambapo kwa kitaifa kwa Zanzibar zilifanyika Chake chake Pemba, (Picha na Haji Nassor, Pemba)

 BAADHI ya wafanyakazi waliohudhuria kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya wafanyakazi dunia, ambapo kitaifa kwa Zanzibar zilifanyika Chake Chake Pemba, wakimsikiliza rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mpinduzi dk, Ali Mohamed Shein wakati akizungumza na wafanyakazi hao mara baada ya kupokea maandamano yao, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
 MWENYEKITI wa vyama vya wafanyakazi Zanzibar ZATUC, dk Zaharan Mohamed Nassor, akitoa hutuba ya kumkaribisha rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi dk Ali Mohamed Shein, kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani ambapo kwa Zanzibar kitaifa, zilifanyika Kisiwani Pemba, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi dk Ali Mohamed Shein akimkabidhi zawadi ya ufanyakazi bora mpiga picha wa Ikulu, Abdalla Haji kwenye maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani, ambapo kitaifa kwa Zanzibar zilifanyika Kisiwani Pemba, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi dk Ali Mohamed Shein akizungumza na mamia ya wafanyakazi wa taasisi za umma na binafsi waliojitokeza kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani, ambapo kwa Zanzibar ilifanyika Kisiwani Pemba, (Picha na Haji Nassor, Pemba).

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.