MKURUGENZI wa Idara ya Maafa Zanzibar, Ali
Juma Hamad akitoa ufafanuzi wa zoezi la Mezani la kukabiliana na maafa, kwa watendaji
wa taasisi za Serikali na binafsi kwa Wilaya ya Wete huko katika Ukumbi wa
Jamhuri Holi Wete.(Picha na Abdi Suleiman, Pemba)
MKUU wa Wilaya ya
Wete Mhe:Hassan Khatib Hassan, akifungua mafunzo ya siku tatu juu Zoezi la Mezani
la Kukabiliana na Maafa Wilaya ya Wete, kwa watendaji wa taasisi za Serikali na
Binafsi wilaya hiyo.(Picha na Abdi Suleiman, Pemba)
WASHIRIKI wa zoezi la
Mezani la Kukabiliana na maafa wilaya ya Wete, washiriki wa kundi la
mawasiliano wakijadilia na mambo mbali mbali, juu la suala la maafa.(Picha
na Abdi Suleiman, Pemba)
SEKRETARI wa Idara ya
Maafa kisiwani Pemba, Maimuna Faki Khamis akigawi chapisho maalumu kwa wakuu wa
taasisi za Serikali na Binafsi, linaloonyesha jinsi gani ya kukabiliana na
maafa yanapotokea.(Picha na Abdi Suleiman, Pemba)
MAKAMANDA Mbali mbali
wa vikosi vya ulinzi na usalama wilaya ya Wete, wakipitia kwa makini chapisho
maalumu linaloonyesha jinsigani ya kukabiliana na maafa yanapotokea.(Picha
na Abdi Suleiman, Pemba)
VIONGOZI wa Taasisi
za Serikali na Binafsi Wilaya ya Wete, wakipitia Chapisho maalumu linaloonyesha
jinsigani ya kukabiliana na maafa yanapotokea.(Picha na Abdi Suleiman, Pemba)
AFISA mdhamini Ofisi
ya Makamo wa Pili wa Rais Pemba, Mhe:Issa Juma Ali akifunga mafunzo ya siku
tatu kwa wakuu wa Taasisi za Serikali na Binafsi juu ya zoezi la Mezani la
kukabiliana na maafa kwa Wlaya ya Wete.(Picha na Abdi Suleiman, Pemba)
No comments:
Post a Comment