WANACHAMA wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii
Zanzibar ZSSF, wakifuatilia mada juu ya mafao ua uzazi, kwenye mkutano wa siku
moja ulioandaliwa na ZSSF na kufanyika jengo la ZSSF mjini Chake Chake Pemba, (Picha na Bakar Mussa, Pemba).
KATIBU Tawala mkoa kusini Pemba, Ahmed
Khalid Abdalla akizungumza na wanachama wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar
ZSSF, juu ya elimu ya mafao ya uzazi, mkutano huo ulifanyika jengo la ZSSF
mjini Chake chake Pemba, (Picha na Haji
Nassor, Pemba).
AFISA uhusiano na masoko wa Mfuko wa
Hifadhi ya Jamii Zanzibar ZSSF, Mussa Yussuf Mussa, akielezea namna mfuko huo
uliovyojipanga kwa ajili ya kutoa mafao ya uzazi kwa wanachama wake, kwenye
mkutano uliojumuisha pia wanachama wa mfuko, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
AFISA Mipango, uwezeshaji na utafiti wa
Mfuko wa hifadhi ya jamii Zanzibar ZSSF, Khalifa Muumini Hilali, akielezea
chimbuko la mafao ya uzazi, kwenye mkutano wa kuelimishwa wanachama juu ya
dhana hiyo, mkutano huo ulifanyika jengo la ZSSF mjini Chake Chake Pemba, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
MDAU wa mfuko wa hifadhi ya jamii
Zanzibar ZSSF ambae hakupatikana jina lake, akiuliza suali kwenye mkutano wa
kuelimishana juu ya mafao ya uzazi, mkutano huo ulifanyika jengo la ZSSF mjini
Chake chake Pemba, (Picha na Haji
Nassor, Pemba).
No comments:
Post a Comment