Habari za Punde

Mahujaji wa Taasisi ya Zanzibar Hajj &Travelling Agency Yawafanyia Semina Mahujaji wao

 
Shekh Khalid Mohammed Mrisho kutoka Kamisheni ya Wakfu na Mali ya Amana Zanzibar akitowa mafunzo kwa Mahujj wa Taasisi Zanzibar Hajj & Travelling Agency, kuhusiana na taratibu za kufuatwa wakati wakiwa Makka kutekeleza Nguzo ya Kiislam ya Hijj wanapokuwa huko semina hiyo imewajumuisha mahujaji wa Taasisi hiyo iliofanyika katika ukumbi wa Bait al Yamin Malindi Zanzibar.
Shekh. Khalid Mohammed Mrisho akisisitiza jambo wakati wa semina hiyo ya Mahujaji ilioandaliwa na Taasisi ya Zanzibar Hajj & Travelling Agency kwa mahujaji wake kutowa mafunzo hayo ya Hija. Kushoto Katibu wa Zanzibar Hajj & Travelling Agency Al Hajj Ali Adam na kulia Mwenyekiti wa Taasisi hiyo Al Hajj Badru Adam.
Waumini wa Kiislamu wanaotarajiwa kwenda Makkah kuhiji wakifuatilia mafunzo hayo yaliyotolewa kwa ajili yao jinsi ya taratibu za Ibada ya Hija wakiwa nchini Saudi Arabia kutekeleza ibada ya Hijja.







No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.