Habari za Punde

Baada ya kumalizika upigaji kura, zoezi la kuhesabu kura limeanza

DSC04102
Afisa wa kituo cha kupigia akibandika bango linaloonesha kuwa ni kituo cha kuhesabia kura baada ya kukamilika kwa zoezi la upigaji kura tarehe 25/10/2015.
DSC04118
Afisa wa kituo cha kuhesabia kura akikata vifungio vya sanduku la kura huku akishuhudiwa na mawakala wa vyama vya siasa kwa ajili ya kuanza zoezi la kuhesabu kura.
DSC04113
Mawakala wa vyama vya siasa vilivyoshiriki Uchaguzi Mkuu wakishuhudia kwa makini zoezi la kuhesabu kura baada ya kukamilika kwa upigaji  wa kura shehia ya Malind Mjini Zanzibar tarehe 25/10/2015.
DSC04121
Afisa wa kituo cha kuhesabia kura Malindi akizimwaga chini Karatasi za kura kwa ajili ya kuanza zoezi la kuhesabu kura.

DSC04123
Maafisa wa kituo cha kuhesabia kura wakihesabu kura za raisi Kwa jumla kabla ya kuzigawanya kwa mujibu wa vyama.
DSC04142
Maafisa wa kituo cha kuhesabia kura shehia ya Saateni wakihesabu kura kwa kuzigawa kwa kila mgombea kwa mujibu wa alivyopata.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.