Habari za Punde

Matukio ya Picha za Watoto Pemba.

 MSAIDIZI mkutubi wa Maktaba kuu ya Chake Chake Pemba Mwache Mohamed Bakari, akiwagawia vitabu wanafunzi wa skuli ya msingi Kiuyu kipangani shehia ya kifundi Jimbo la Konde Wilaya ya Micheweni, ikiwa ni lengo la uhamasihaji wanafunzi wa skuli za msingi kupenda kusoma vitabu, katika utekelezaji wa mradi wa Out Reach Program unaofadhiliwa na SIDA.
 MWANAFUNZI Fatma Ahmed Omar anayesoma darasa la sita katika skuli ya msingi Kiuyu Kipangani shehia ya Kifundi Jimbo la Konde Wilaya Micheweni, akisoma risala ya usomaji wa vitabu katika utekelezaji wa mradi wa Out Reach Program unaofadhiliwa na SIDA
 MSAIDIZI mkutubi wa maktaba kuu ya Chake Chake Pemba, Mwache Mohamed Bakari akiwaimbisha nyimbo wanafunzi wa skuli ya msingi Kiuyu Kipangini shehia ya Kifundi Jimbo la Konde Wilaya ya Micheweni, wakati wa utekelezaji wa mradi wa Out Reach Program unaofadhiliwa na SIDA.
 MSAIDIZI mkutubi wa maktaba kuu ya Chake Chake Pemba, Mwache Mohamed Bakari akiwaonesha wanafunzi wa skuli ya Msingi Kiuyu Kipangani, jinsi gani ya usomaji wa kitabu wakati wa utekelezaji wa mradi wa Out Reach Program Unaofadhiliwa na SIDA.
 MWANAFUNZI Seif Khatib Mtwana akisoma taarifa ya skuli yake ya Kiuyu Kipangani jinsi inayotoa huduma za maktaba, wakati wa utekelezaji wa mradi wa Out Reach Program unaofadhiliwa na SIDA.

 MSAIDIZI mkutubi wa maktaba Kuu Chake Chake Pemba, Mwache Mohamed Bakari akiwaonyesha wanafunzi wa skuli ya msingi Kiuyu Kipangani picha mbali mbali zinazopatikana maktba za Pemba, wakati wa utekelezaji wa mradi wa Out Reach Program unaofadhiliwa na SIDA.
 MWANAFUNZI Asha Khamis akitoa kitandawili kwa wenzake wakati wa uhamasishaji wanafunzi kutumia makataba katika utekelezaji wa mradi wa Out Reach Program Unaofadhiliwa na SIDA
 MWANAFUNZI Saumu Rashid Haji wa darasa la kwanza katika skuli ya Kiuyu Kipangani, akijibu chemsha bongo wakati wa uhamasishaji wanafunzi kutumia maktaba katika utekelezaji wa mradi wa Out Reach Programa unaofadhiliwa na SIDA.
 MWANAFUNZI Subira Khalid Omar akisoma hadithi katika kitabua wakati wa uhamasishaji wanafunzi kutumia maktaba kwenda kujisomea, katika utekelezaji wa mradi wa Out Reach Program unaofadhiliwa na SIDA
WANAFUNZI wa skuli ya msingi Kiuyu Kipangani shehia ya kifundi jimbo la Konde, wakichora picha mbali mbali katika utekelezaji wa mradi wa Out Reach Program unofadhiliwa na SIDA.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.