Habari za Punde

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Ziarani Kisiwani Pemba

 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kusini Pemba Shehan Mohammed Shwhan akizungumza wakati wa Ziara ya Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe Hamad Yussuf Masauni, akiwa katika ziara yake Kisiwani Pemba kujitambulisha na kuangalia utendaji wa Jeshi huilo Kisiwani Pemba. 
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani akizungumza na waandishi wa habari wakati wa ziara yake kisiwani Pemba ikiwa ni kujitambulisha kwa Makamanda wa Polisi kisiwani humo na kupata taarifa za utendaji wa kazi zao za kila siku. 
Kamishna wa Polisi Zanzibar Hamdan Omar Makari akijibu na kutoa ufafanuzi wa maswali yaliolizwa wakati wa ziara ya Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Kisiwani Pemba.
Askari wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kusini Pemba wakimsikiliza Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe Hamad Yussuf Masauni akizungumza na wapiganaji hao wakati wa ziara yakew mkoa wa Kusini Pemba kujitambulisha na kupata utendaji wa kazi za Jeshi la Polisi Pemba. 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.