Habari za Punde

Hutuba ya Waziri wa Fedha Zanzibar Omar Yussuf Mzee Wakati wa Ufunguzi wa Tawi la Bank Of Africa Zanzibar

HOTUBA YA MHESHIMIWA OMARI YUSUF MZEE, WAZIRI WA FEDHA WA SERIKALI YA MAPINDUZI ZANZIBAR, KATIKA SHEREHE ZA UFUNGUZI WA TAWI JIPYA LA BANK OF AFRICA TANZANIA- ZANZIBAR TAREHE 3 MACHI 2016

Balozi Mwanaidi Sinare Maajar, Mwenyekiti wa Bodi ya 

Wakurugenzi wa BANK OF AFRICA - TANZANIA

Ndugu Ammish Owusu-Amoah, Mkurugenzi mtendaji wa 

BANK 

OF AFRICA - TANZANIA;

Wakurugenzi wa Bodi;

Wafanyakazi wa BANK OF AFRICA - TANZANIA;

Wageni waalikwa;

Ninayo furaha kubwa kuwa nanyi leo wote mliojumuhika 

hapa kushiriki katika sherehe hii ya uzinduzi wa Tawi jipya la 

BANK OF AFRICA ZANZIBAR. Nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa siku hii njema na kwa kutupa uwezo wa kuwa hapa leo. Napenda kuwashukuru pia viongozi wote wa BANK OF AFRICA kwa kunipa heshima hii kubwa ya kuzindua Tawi hili siku hii ya leo. Kwa dhati kabisa nawapongeza wote walioshiriki katika mchakato mzima wa kufanya tathmini na hatimaye kuamua kufungua Tawi la BANK OF AFRICA hapa Zanzibar. 

Kipekee nawashukuru Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi, Balozi Mwanaidi Sinare Majaar na   Mkurugenzi Mtendaji wa Benki, Bwana Ammish Owusu- Amoah kwa jitihada zao kubwa za kutoa msukumo wa kuanzishwa kwa Tawi hili. Nawashukuru na kuwapongeza wote. Nitumie nafasi hii pia kuwapa hongera wananchi wa Zanzibar kwa kupata tawi la BANK OF AFRICA. Hongereni sana!


Leo ni siku adhimu na ya kipekee ambapo tunashuhudia ufunguzi wa Tawi hili jipya la BANK OF AFRICA ambalo litakuwa Tawi la kwanza hapa Zanzibar. Ni dhahiri kwamba ufunguzi wa Tawi hili ni ishara kwamba BANK OF AFRICA - TANZANIA imedhamiria kupanua shughuli za kibenki nchini hasa katika kukuza uchumi wa Zanzibar. 

BANK OF AFRICA inakuja na mengi mpya katika Sekta ya Benki na kuleta huduma za kibenki karibu na wananchi wa Zanzibar ikiungana na Benki zingine pamoja na kushirikiana na BENKI KUU YA TANZANIA.

Wageni waalikwa,

Serikali inatambua kwamba maendeleo yetu hususan ya kukuza uchumi na kuondoa umaskini hayawezi kuwa na mafanikio bila ya kuhusisha Sekta binafsi. Hii ndiyo sababu katika miaka ya 1980 Serikali ilifanya juhudi kubwa katika kubadili Mfumo wa Uchumi kutoka Mfumo Hodhi wa Dola kwenda Mfumo wa Soko Huria. 

Katika mabadiliko hayo pia kulifanyika mageuzi katika Sekta 

mbalimbali ikiwemo Sekta ya Fedha. Uamuzi wa BANK OF 

AFRICA - TANZANIA kuwekeza kwenye upanuzi wa huduma

zake hapa Zanzibar, ni utekelezaji thabiti wa dhamira ya Serikali ya kuvutia uwekezaji wa ndani na nje ili kukuza Uchumi kwa kasi zaidi.

Vilevile, tumekuwa tukifanya mageuzi mbalimbali tangu miaka ya1990 kwa mtazamo wa kuiwezesha Sekta Binafsi kuwa ya muhimu sana katika Ukuaji wa Uchumi wetu. Katika miaka ya hivi karibuni Serikali inajivunia kwamba tangu kuingia kwa Mfumo wa Soko Huria hapa Nchini, Sekta Binafsi imeweza kuchukua nafasi yake na kuwekeza katika huduma mbalimbali zikiwemo huduma za Sekta ya Fedha. 


Serikali itaendelea kuhakikisha uhusiano wa karibu uliopo kati ya Serikali na Sekta Binafsi zikiwemo Taasisi za Fedha unakuwa uhusiano wa kudumu. Tutaendelea kuheshimu mchango wa Sekta Binafsi ambao ni kichocheo kikubwa kwa Uchumi na maendeleo ya Taifa letu. Serikali itaendelea na jukumu lake la kuboresha mazingira ya uwekezaji ili kuhamasisha wawekezaji zaidi Nchini.

Pamoja na jitihada hizo bado kuna maeneo yanayohitaji kuboreshwa ili kujenga mazingira bora ya Sekta Binafsi kukua hasa suala la upatikanaji wa huduma za Kibenki Vijijini na katika Sekta ya Kilimo. Nafurahi BANK OF AFRICA mmeanza vizuri kuisaidia Serikali kuleta maendeleo katika huduma za Benki hapa Zanzibar.

Wageni waalikwa,

Napenda kuwahakikishia kwamba serikali inafanya kila iwezalo katika kuhakikisha huduma za kifedha zinamfikia kila Mzanzibari kwa urahisi kabisa. Katika kuhakikisha hili linafanyika serikali ya Zanzibar inafanya ujenzi na uboreshaji wa miundombinu hasa barabara, njia za mawasiliano na utengenezaji wa Sera zilizo stahiki.

Hii ni pamoja pia na kupigana na umasikini na ukosefu wa 

elimu kwa wananchi wa Zanzibar.

Nimekuwa nikiangalia na pia kutokana na maelezo niliyopewa na Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugeni, ni kwamba katika miaka hii tisa BANK OF AFRCA imekuwa na uwezo wa kufungua matawi 22 sasa pamoja na Tawi maalum kwa ajili ya wateja wakubwa pale Dar es Salaam.

Pamoja na hili utaona kwamba matawi mengine yameenda ndani zaidi katika maeneo ambayo upatikanaji wa huduma za kibenki ni adimu. Benki imetengeneza huduma za kipekee zakumfaa kila mmoja wetu ambazo pia zinapunguza ugumu wa utumiaji wa huduma za kibenki kwa watu binafsi,wenye biashara ndogondogo, wenye vikundi, wafanyabiashara za 
kati na hata wafaya biashara wakubwa.

Wageni waalikwa,

Sasa ni wakati wa Zanzibar kutumia huduma hizi zinazotolewa na BANK OF AFRICA, ili kupata maendeleo yale tunayoyahitaji. 

Wazanzibari hizi ndizo fursa, tusizifumbie macho. Wale 
wakulima,wavuvi, wenye mahoteli, wafanya biashara na vijana, sasa ni wakati wa kutumia fursa hizi.

Nimeambiwa kwamba Tawi limepata mapokezi ya kipekee kutoka kwa watu wa Mlandege na natumaini kwamba heshima ambayo benki imejijengea katika miaka yake tisa ndani ya Tanzania bara itaenea pia Zanzibar. Na pia natumaini Zanzibar hatutobaki na tawi hili moja la BANK OF AFRICA bali yataongezeka matawi mengi zaidi.

Wageni waalikwa,

Niombe uongozi pamoja na wafanyakazi wote wa BANK OF 

AFRICA kuhakikisha kwamba wateja wa Tawi hili la Zanzibar

wanapata huduma za kipekee katika viwango vya kimataifa 

tukiweka pamoja na mahitaji ya Wazanzibari katika benki yenu. 

Natumaini kuwa una wafanyakazi wenye sifa, uwezo na weledi wa kufanya kazi na hivyo unachohitaji sasa ni wateja.

Kwa haya machache, kwa niaba ya Serikali ya Mapinduzi ya 

Zanzibar, naomba nichukuwe nafasi hii kufungua rasmi na 

kutambua Tawi jipa la BANK OF AFRICA ZANZIBAR.

Niwashukuru tena wote kwa kuhudhuria tukio hili la kihistoria 

kwa Zanzibar na nawakaribisha wote kuwa wateja wa BANK 

OF AFRICA.


Asante. 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.