DW kutengeneza
video zenye habari kwa Kiswahili
Idhaa ya Kiswahili ya DW imeanzisha huduma mpya: Mukhtasari
wa habari ndani
ya sekunde 100. Mbali na kukuletea matangazo ya
redio ya kila siku kwa ajili ya
Afrika Mashariki na eneo la Maziwa
Makuu, Jumatatu hadi Ijumaa DW itakupatia
video fupi zenye
habari. Mkuu wa Idhaa ya Kiswahili, Andrea Schmidt, ana furaha
kwamba yeye na timu yake ya waandishi wa habari kutoka nchi
tano tofauti
wanaanzisha huduma hii mpya itakayoitwa “Papo kwa
Papo” na
itakayokuwa jicho la kuutazama ulimwengu. Kupitia
video zetu utaweza kupata
habari muhimu za kimataifa za kila siku.
“Papo kwa Papo” itapatikana katika chaneli ya YouTube ya DW
Kiswahili,
Facebook na toleo fupi la sekunde 60 litarushwa kupitia
WhatsApp.
Miongoni mwa mambo mengine, tutakuletea “hashtag” zilizovuma
pamoja na
katuni za kisiasa kutoka kwa wasanii maarufu Gado na
Said Michael.
Pamoja na hayo, kila Ijumaa DW Kiswahili itakuletea sekunde 100
za matukio
muhimu ya kisiasa yaliyotokea katika juma zima.
·
Tafadhali kuwa shabiki wetu YouTube: www.youtube.com/kiswahili
·Jiunge nasi katika ukurasa wetu wa Facebook: https://www.facebook.com/dw.kiswahili.
·
Pata “Papo kwa Papo” na taarifa zaidi kupitia
WhatsApp. Unaweza
kujiunga nasi kupitia kiungo hiki: bit.ly/1Q86kjt
Kila siku Idhaa ya Kiswahili ya DW inarusha masaa matatu ya
matangazo
Afrika Mashariki na katika eneo la Maziwa Makuu.
Kwa kushirikiana na redio
washirika katika eneo zima, DW
inawapatia wasikilizaji habari zisizoegemea
upande wowote
kuhusu yanayojiri duniani kwa ujumla na hasa barani Afrika
kupitia
masafa ya FM. Ili kutoa mtazamo huu wa kimataifa, timu
ya waandshi wa habari
kutoka nchi tano inafanya kazi na mtandao
mkubwa wa waandishi walioko Afrika na
kwengineko.
Matangazo ya Kiswahili ni miongoni mwa matangazo ya DW
yenye wasikilizaji
wengi zaidi. DW inajumuisha vipindi
vilivyopokea tuzo kama vile Learning by Ear
- Noa bongo, jenga
maisha yako - na vipindi vinavyojadili afya, haki za
binadamu,
mazingira, wanawake na maendeleo, vijana na utamaduni na sanaa.
www.dw.com/kiswahili
No comments:
Post a Comment