Zanzibar,
19, Aprili-2016: Kampuni ya simu inayoongoza
visiwani Zanzibar, Zantel imetoa msaada wa kompyuta 21 na huduma ya intaneti bure kwa vyuo saba
vya walimu pamoja na shule ili kuboresha na kukuza mfumo wa elimu kupitia mafunzo ya habari na teknolojia ya maswasiliano .
Msaada huo wenye thamani ya shilingi milioni 34
umetolewa wiki moja tu baada ya kampuni hiyo kuzindua mtandao wa kasi wa 4G
pamoja na kutanua upatikanaji wa mtandao upande wa bara.
Kompyuta hizo ambazo zimeunganishwa na mtandao wa
inteneti kwa muda wa miezi mitatu zitasaidia kukabiliana na uhaba wa walimu wenye
ujuzi katika teknolojia ya mawasiliano
visiwani Zanzibar.
Vyuo na shule zitakazo
pokea msaada huo ni pamoja na chuo cha biashara cha Zanzibar (Unguja), shule ya
Chasasa (Pemba), chuo cha taifa cha Ualimu (Unguja),Chuo cha Ualimu Kiembe Samaki (Unguja),chuo cha ualimu cha Michakaeni
(Pemba), chuo ch Ualimu ( Unguja) na chuo cha
Ualimu Kitogani (Unguja).
Akizungumza wakati wa
makabidhiano hayo, Afsa Mtendaji
Mkuu wa kampuni ya simu ya Zantel, Bwana Benoit Janin alisema lengo la Zantel ni
kushirikiana na serikali kwa lengo la kukuza na kuboresha elimu ya teknolojia
na mawasiliano na kusaidia vyuo vya
ualimu vinayotoa mafunzo hayo ili kuongeza ufanisi katika ufundishaji wao.
'Ni matumaini yetu mchango huu utasaidia kuendeleza
elimu ya teknolojia na mawasiliano na kuwanufaisha walengwa kwa kuwawezesha
kutekeleza majukumu yao na kuongeza wataalamu
kwenye taifa' alisema Janin.
Akizungumza wakati wa tukio hilo, Mkurugenzi wa bodi wa Zantel na Afsa Mtendaji
wa Millicom Africa, Bi Cynthia Gordon alisema walimu ndio msingi wa maendeleo
kwenye taifa na ndio maana Zantel imewapa kipaumbele katika miradi yake ya
kijamii.
'Daima Zantel tumekuwa mstari wa mbele katika
kuhakikisha tunaboresha sekta ya elimu kwa wazanzibari na kama tunavyojua elimu
ya teknolojia na mawasiliano ni muhimu kwa dunia ya sasa ' alisema Bi Gordon.
Katika hotuba yake, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya
Ufundi, Mheshiwa Riziki Pembe Juma, ameipongeza kampuni ya Zantel kwa jitihada zake inayofanya kwa kushirikiana na serikali katika
kukuza na kuboresha elimu visiwani Zanzibar.
'Ili kutoa elimu bora kwa walimu wa teknolojia ya
mawasiliano wa ngazi zote ni muhimu kuhakikisha mafunzo ya komputa
yanajumuishwa kwenye mtaala wa vyuo vya elimu ili kuwajengea uwezo walimu
katika kufundisha wanafunzi' alisema Mheshimiwa Riziki Pembe Juma.
Zantel imekuwa ikitoa michango mbalimbali kwenye sekta
ya elimu visiwani Zanzibar ikiwemo kusaidia ununuzi wa vitabu kwa maktaba kuu
ya Zanzibar na pia kutoa msaada kwenye shule za msingi kama vile Kisiwandui na pia
ukarabati wa madarasa katika shule ya Mikanyageni mkoani Pemba.
No comments:
Post a Comment