Habari za Punde

Mradi wa Ujenzi wa Nyumba za Kisasa Fumba

Managing Director wa Mradi wa Nyumba za Kisasa Fumba Zanzibar, Sebastian Dietzold,akitowa maelezo ya Mradi huo wa Ujunei wa Nyumba za Kuishi kwa Bei Nafuu katika maeneo huru ya Biashara Fumba Zanzibar. kwa waandishi wa habari Zanzibar katika ukumbi wa hoteli ya Zanzibar Ocean View Kilimani Zanzibar.
Managing Director Mradi wa Nyumba za Kisasa Fumba Sebastian Dietzold, akitowa maelezo ya maendeleo ya Ujenzi wa Nyumba hizo zinazoendelea kujengwa katika maeneo ya Fumba Zanzibar na kuuzwa kwa bei nafuu kwa Wananchi, akisisitiza maendeleo ya mradi huo unavyoendelea vizuru na tayari wameshajenga nyumba nyingi na kiziuza kwa Wananchi kwa bei nafuu.
Mkurugenzi akisisitiza jambo wakati akizungumza na Waandishi wa habari maendeleo ya mradi huo na mafanikio yake katika ujenzi huo, 
Waandishi wa habari wakifuatilia maelezo ya Mradi wa Ujenzi wa Nyumba za Kisasa katika maeneo huru ya Fumba Zanzibar.



3 comments:

  1. Nyumba hizi si za bei nafuu, hivi dola 50,000/ ambazo karibu sawa na milioni Mia moja, inakuwaje bei rahisi kwa mzanzibari wa kawaida?

    ReplyDelete
  2. watu washatiwa jiti hapo, kuna jamaa wanasema hapo kuna mchezo mchafu wanataka kuwaibia wazanzibari wanaoishi nje, hizo sio kwa wanaoishi hapo

    ReplyDelete
  3. Kila mtu ambaye anataka kupata maelzo zaidi na sahihi tunamkaribisha sana ofisi yetu (CPS Live Ltd.) Mazizini Zanzibar. Saa za kazi ni saa 3 asubuhi hadi saa 11 jioni, Jumatatu - Ijumaa.

    ReplyDelete

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.