Habari za Punde

Zanzibar Press Club Yaadhimisha Siku ya Uhuru wa Vyombo Habari kwa Kongamano la Waandishi Zanzibar.

Katibu wa Zanzibar Press Club Ndg Mwinyimvua akizungumza wakati wa Kongamano la Waandishi wa Habari Zanzibar kuadhimisha Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani huadhimishwa kila mwaka 3 Mei, maadhimisho hayo yamefanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Zanzibar Ocean View Kilimani Zanzibar.
Mwenyekiti wa Zanzibar Press Club Ndg Abdulla Abdurahaman akizungumza na waandishi wa habari wa Zanzibar wakati wa Kongamano la kuadhimisha Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani lililowashirikisha Waandishi wa Habari wa Vyombo mbalimbali vya Serikali na Binafsi, lililofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Zanzibar Ocean View Kilimani Zanzibar.
Waziri wa Kilimo Maliasili Mifugo na Uvuvi Mhe. Hamad Rashid Mohammed akifungua Kongamano wa Waandishi wa Habari kuadhimisha Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani lililofanyika katika ukumbi wa hoteli ya Zanzibar Ocean View Kilimani Zanzibar, na kuwataka waandishi wa habari kufuata maadili ya Kazi zao wanaporipoti habari kwa Wananchi bila ya kuwa na upendeleo wanapotoa taarifa kwa Wananchi, Waandishi ni kioo cha jamii na kuelimisha.    
Mhe Hamad Rashid Mohammed akisisitiza jambo wakati wa hutuba yake ya Ufunguzi wa Kongamano la Waandishi wa Habari Zanzibar kuadhimisha Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani lililofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Zanzibar Ocean View Kilimani Zanzibar.
Waandishi wakiwa makini kusikiliza hutuba ya mgeni rasmin Waziri wa Kilimo Maliasili Mifugo na Uvuvi Mhe Hamad Rashid Mohammed ikiwa ni Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani huadhimishwa kila mwaka 3 Mei. 
Waandishi wakimsikiliza Mgeni rasmin akitowa nasaha zake kwa Waandishi wa Habari wakati swa Ufunguzi wa Kongamano la Uhuru wa Vyombo vya Habari, lililoandaliwa na Zanzibar Press Club katika ukumbi wa Hoteli ya Zanzibar Ocean View Kilimani Zanzibar.
Mkuu wa Chuo cha Waandishi wa Habari Zanzibar Dk Abubakar Rajab,akitowa Mada katika Kongamano hilo la kuadhimisha Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani Akiwasilisha Mada yaMiaka 22 ya Azimio la Windhoek (Namibia) Kuhusu Uhuru wa Vyombo vya Habari. Wajibu wa Mamlaka za Umma Kustawisha Uhuru wa Vyombo vya Habari Kama Nyenzo ya Kukuza Utawala Bora na Uwajibikaji Nchini ( Zanzibar) 
22 Anniversary of Windhoek (Namibia) Declaration on Freedom of Press : Public



















No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.