Habari za Punde

Waziri Aboud Azindua Baraza la Vijana swa Shehia 12 za Jimbo la Kikwajuni Zanzibar Viwanja vya Mnara wa Kumbukumbu ya Mapinduzi Michezani Kisonge.

Wasanii wa muziki wa Kizazi Kipya wa Dansa FB wakitowa burudani wakati wa uzinduzi wa Mabaraza ya Vijana Jimbo la Kikwajuni Zanzibar katika viwanja vya Mnara wa Kumbukumbu ya Mapinduzi Michezani Kisonge Zanzibar.
Kikundi cha Vijana wa Jimbo la Kikwajuni wakicheza ngoma ya Danedane sale wakati wa Uzinduzi wa Baraza la Vijana Jimbo Kikwajuni lililojumuisha Shehia 12 za jimbo hilo
Vijana wa Kikundi cha Ngoma cha Danedane Sare wakitowa burudani wakati wa Uzinduzi wa Baraza la Vijana Jimbo la Kikwajuni Zanzibar.
Vijana wa Jimbo la Kikwajuni wakinadisha picha hya kuchora ya Muasisi wa Mapinduzi ya Zanzibar Marehemu Mzee Abeid Amani Karume wakati wa Mnada wa Uzinduzi huo wa Baraza la Vijana Jimbo la Kikwajuni picha hiyo imenunulia shilingi laki mbili na nusu katika mnada huo.
Mgeni rasimin katika hafla ya Uzinduzi wa Baraza la Vijana Jimbo la Kikwajuni Zanzibar,Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe Mohammed Aboud Mohammed, akimkabidhi mnunuzi wa picha hiyo Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Kazi Uwezeshaji Wazee Vijana Wanawake na Watoto Bi. Maua Makame Khamis .
Mgeni rasimin katika hafla ya Uzinduzi wa Baraza la Vijana Jimbo la Kikwajuni Zanzibar,Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe Mohammed Aboud Mohammed, akimkabidhi mnunuzi wa picha hiyo Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Kazi Uwezeshaji Wazee Vijana Wanawake na Watoto Bi. Maua Makame Khamis, kulia Mwenyekiti wa Mabaraza ya Vijana Jimbo la Kikwajuni Amina Ali Mzee.
Kijana wa Jimbo la Kikwajuni Hilal Hussein akisoma risala wa Mabaraza ya Vijana wa Jimbo la Kikwajuni wakati wa Uzinduzi huo uliofanyika viwanja vya Mnara wa Kumbukumbu Michezani Kisonge Zanzibar.
Viongozi wa Meza Kuu wakisikiliza risala ya Vijana wa Mabaraza ya Jimbo la Kikwajuni Zanzibar wakati wa uzinduzi huo.
Mwenyekiti wa Mabaraza ya Vijana Jimbo la Kikwajuni Amina Ali Mzee. akihutubiwa wakati wa uzinduzi huo na kumkaribisha Mkuu wa Wilaya ya Mjini. 
Katibu Mtendaji wa Baraza la Vijana Ndg Khamis Faraji akihutubia na kutowa nasaha zake kwa Vijana wa Jimbo la Kikwajuni wakati wa uzinduzi wa Baraza la la Vijana katika Viwanja vya Mnara wa Kumbukumbu Michezani Kisonge Zanzibar na kumkaribisha Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Vijana.


















No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.