Na Evelyn Mkokoi. Dar es Salaam.
Kiwanda nda cha kutengeneza vyuma cha MMI Steel kilichopo katika
eneo la viwanda mikocheni jijini Dar es Salaam, kimetozwa faini ya shilingi
milioni kumi na kutakiwa kulipa faini hiyo baada ya siku saba kwa kosa la
kukiuka sheria ya mazingira na kanuni zake ya mwaka 2004, kwa kutiririsha maji
machafu katika maeneo ya mtaa wa TPDC kwa warioba jijini dar es salaa. Maji ambayo
ni hatari kwa mazingira na viumbe hai.
Adhabu hiyo imetolewa na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa
Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina alipotembelea eneo la mtaa wa viwanda mikocheni kufuatia uchafuzi
wa mazingira unaotokanao na utitiririshaji wa majitaka katika maeneo hayo.
Wakati huohuo, Shirika la maji safi na majita taka Jijini Dar
es
Salaam na Pwani ( Dawasco) limepewa siku
kumi na saba
kumaliza tatizo la utiririshaji wa maji taka katika mtaa wa TPDC
mikocheni kwa Warioba jijini Dar es Salaam.
Maagizo hayo yametolewa na Naibu Waziri Mpina Baada ya
kufanya usafi jumamosi ya mwisho wa mwezi wa tatu na kutoa
siku saba kwa
DAWASCO na NEMC kusimamia suala zima la
usafi wa mazingira na agizo lake
kuupuzwa.
Awali, Mhe. Mpina alisema kuwa uchafuzi wa mazingira hauwezi
kuendelea kuvumiliwa na lazima hatua za kisheria zichukuliwe, na
kuwaasa
watendaji wa taasisi za serikali kuyapa kipaumbele
maagizo yanayotolewa na
viongozi wa ngazi za juu za serikali
kinyume na hapo ni kutokutii mamlaka.
“tasisi za serikali lazima
zifanye kazi kwa kushirikiana kutokana na kwamba
kumekuwa na
kutupiana mpira kati ya NEMC, dawasco na Manispaa ya
kinondoni
katika suala zima la utatuzi wa uchafuzi wa mazingira
katika mtaa wa TPDC.”
Alisema.
Naibu waziri Mpina aliongeza kuwa ifikapo tarehe 30/7/2016
asikutane tena na tatizo la uchafu na harufu
mbaya katika mtaa wa
TPDC kwani hali hiyo ni hatari sana kwa afya ya wakazi wa
maeneo hayo na mazingira.
Kwa upande wake DAWASCO ikiwakilishwa na Injinia Erick
Jackson alisema kuwa Tangu muheshimiwa Naibu Waziri Mpina
atoe agizo la
uondoshwaji wa majitaka na uboreshwaji wa
miundombinu katika mtaa huo, wamekuwa
wakifanya kazi na
bado inaendelea na kazi hiyo pamoja na kukabiliwa na changamoto mbalimbali
za kifedha na ufundi.
Hata hivyo uongozi wa Halmashauri ya wilaya ya kinondoni
umelishitaki shirika la maji safi na maji taka jijini dar es salaam na
Pwani
DAWASCO ,kiwanda cha MMI steel na Tembo Tiles kwa
uchafusi wa mazingira kwa
kutirirsha maji taka.
No comments:
Post a Comment