Habari za Punde

Mkuu wa Wilaya ya Lindi Aahidi kusimamia Ujenzi wa shule ya Sekondari Lindi Hadi Kukamilika

Na: Mwandishi Wetu.
Mkuu wa Wilaya ya Lindi Mheshimiwa Shaibu Issa Ndemanga, leo ametembelea katika Shule ya Sekondari ya Lindi iliyopo katika manispaa ya lindi mjini kwa lengo la kuanza ujenzi wa shule hiyo ikiwa ni agizo la Waziri mkuu Kassimu Majaliwa ambaye aliitembelea shule hiyo ivi karibuni baada ya kuungua Moto na kuteketeza zaidi ya madarasa 8 katika shule hiyo.

Mkuu huyo wa Wilaya ambaye ameanza utendaji wake kwa kasi ikiendana na Kasi ya serikali ya awamu ya tano chini ya Rais wa jamhuri ya Muungano John Pombe Magufuli, aliitembelea shule hiyo kwa lengo la kuangalia changamoto zilizopo ikiwa ni pamoja na kujadili suala la Ujenzi wa barabara itakayotumika kwa ajili ya kuhakikisha vifaa vya ujenzi wa shule vinafika kwa usalama katika eneo hilo la madarasa wakati huu ambapo ujenzi unatarajiwa kuanza mara moja.

Akizungumzia ujenzi wa shule hiyo Mkuu huyo wa  Wilaya ya Lindi  Mjini alisema kuwa analazimika kufuatilia suala hilo lifanyike kwa haraka kutokana na kuwa agizo lililotolewa na Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa alipotembelea shule hiyo wakati wa uchangiaji wa harambee kwa alengo la kufanikisha ujenzi huo kupitia wadau mbalimbali waliochangia Ujenzi wa Shule hiyo.

“Siyo jambo la taratibu hili, maana ni maagizo ambayo yametolewa na Mheshimiwa Waziri Mkuu kwamba ufanyike kwa haraka iwezekanavyo, kwa hiyo mimi nafuatilia kutimiza Kauli ya Waziri Mkuu ambaye alisimamia uhamasishwaji wa uchangiaji wa ujenzi wa majengo ya Shule yalioungua kwa Moto, na kama unavyoona mwenyewe tayari wadau wameendelea na zoezi la kutoa kile walichosema watatoa, na hapa leo nakagua kwanza Sehemu ya Barabara ambayo itajengwa kwa dharura ili kufikisha Vifaa eneo la Ujenzi lakini si hivyo tu hapa kuna changamoto nyingi ambazo zinatakiwa kufanyiwa ufumbuzi ikiwa ni pamoja na kupata mchoro wa jingo ambao unatakiwa uandaliwe kwa haraka na siyo vinginevyo, pili ni kwa hawa wajenzi ambao wanatakiwa kubuni barabara mbadala ambayo pamoja na kwamba itatumika kwa ujenzi huu lakini pia iwe ni barabara ambayo itakuwa ya kudumu kwa lengo la kuja kusaidia wakati mwingine kama itatokea tatizo kama hili, kitu kingine ni jinsi ambavyo wajenzi wanatakiwa kubuni mchoro wenye kiwango kwa ajli ya kuendana na dunia ya sasa, siyo tu bora mchoro, wahakikishe mchoro huo unakuwa kivutio na jingo lenyewe liwe ni jingo linalokidhi mahitaji kwa ajili ya shule hii, pamoja na kwamba changamoto ni nyingi lakini pia nimefika hapa kuangalia kile ambacho tayari kimepatikana na wapi kimehifadhiwa, si unajua unaweza kupata lakini ukose sehemu ya kuhifadhi, tunatarajia kupokea mifuko ya Simenti kutoka Dangote zaidi ya 4000 na mabati kama 400 ivi kwa hiyo ni lazima nifahamu ni wapi itakuwa stoo ya kuifadhi hivyo vifaa, na nataka kusimamia mimi mwenyewe ujenzi huu kwa haraka ili kutimiza maagizo ya Waziri Mkuu “ alisema Ndemanga

Na kuongeza kwamba ujenzi huo tayari umeanza rasmi na hivyo zoezi la kwanza ni kuangalia jinsi ambavyo  utaratibu wa kubomoa majengo yaliyoungua na uzoaji wa vifusi utakavyofanyika na wakandarasi bila kuathili shuguli za kimasomo za wanafunzi wanaoendelea na shuguli zao za kimasomo hapa  shuleni.

Katika Ziara hiyo ya ukaguzi wa maeneo ya ujenzi Mkuu wa Wilaya alifuatana na Mkurugenzi wa Manispaa ya Lindi Mjini  Bwana  Jomaary Mrisho Satura, pamoja na Mkandarasi wa Majengo aliyekabidhiwa ujenzi huo wa majengo ya shule  hiyo ya Lindi Sekondari  Engeneer Lusekelo Mwakyami ambao kwa pamoja  waliweza kushirikiana kimawazo kushauriana na Mkuu huyo wa Wilaya kuangalia maeneo ambayo kunatakiwa Barabara ipite, ikiwa ni pamoja na kushauliana kuhusu Nguzo za tanesco zilizopo maeneo hayo ya ujenzi wa Majengo ya Shule, Mitaro iliyopo kwa ajili ya kupitisha maji wakati mvua zinaponyesha , pamoja na kuangalia maeneo ya viwanja vya michezo ili yasijekuharibiwa na ujenzi huo.
Aidha waliweza kushauriana pia namna ambavyo kwenye ujenzi huo ambayo utakuwa wa ghorofa na siyo ujenzi wa madarasa ya chini, kuangalia jinsi ambavyo wachoraji wa ramani wanatakiwa kuweka njia za magari ambayo yatapita hadi eneo la wazi au kuweka parking za magari ya viongozi na siyo tu kuishia mbali kama ilivyokuwa hapo awali.
“tunafikilia kuwa jingo hili ambalo ni ghorofa liwe na maeneo ya parking za magari, yaani magari yawekewe njia za kupita, naamini kwamba  katika majengo haya kutakuwa na idadi kubwa za maofisi ya walimu pamoja na kwamba kutakuwa na madarasa pia, hivyo walimu ambayo watakuwa na vyombo vyao vya usafiri au magari ya serikali yaweze kuingia hadi maeneo haya ya Majengo kwa ndani, maana majengo haya tunatarajia kwamba yatakuwa ya kisasa nay a kupendeza na yatakayokuwa yameendana na duania ya sasa, na ndiyo maana umetuona sisi wote, Kaimu mkuu wa Mkoa, ambaye ni DC wetu, mkandarasi wa Manispaa na mimi Mkurugenzi wote tumefika ili kujadiliana kwa umakini suala hili ili baada ya ujenzi kusipo na maswali kutoka kwa wakuu wetu” alisema Satura
 Kwa mujibu wa Mkuu wa Wilaya mheshimiwa Shaibu Ndemanga, alisema kuwa yeye mwenyewe atakuwa ni mionmgoni mwa wajenzi wa majengo kutokana na kwamba ni wajibu wake kuhakikisha kila siku anawasili kukagua hatua kwa hatua hadi ujenzi utakapokuwa umekamilika.

Ivi karibuni Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa wakati wa Ziara yake mkoani lindi alitoa agizo la kuharakishwa ujenzi wa shule hiyo huku yeye mwenyewe akiwa ni miongoni mwa viongozi waliofika wakati wa uchangiaji wa harambee ya kuhakikisha kiasi cha fedha kinapatikana kutoka kwa wadau mbali mbali wa Elimu wa mkoa wa lindi kwa lengo la kufanyika kwa ujenzi wa shule hiyo.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.