Habari za Punde

Nafasi za masomo ya Uimamu na Ualimu wa Madrasa nchini Algeria

Kamisheni ya Wakf na Mali ya Amana Zanzibar inawatangazia nafasi za masomo ya Uimamu na Ualimu wa madrasa chini Algeria  kwa muda wa miaka 3 kwa ngazi  ya diploma na digrii . 

Sifa za muombaji 
1. Awe amehitimu kidato cha nne. 
2. Awe anajua kusoma  na kuandika kwa lugha  ya Kiarabu kwa ngazi diploma na kwa ngazi digirii awe amehetimu  kwa ngazi ya shahada ya mwanzo na sifa nyengine zilotajwa hapo juu 
3. Barua ya maombi iambatanishwe na vivuli vya vyeti vifuatavyo:-  
1. Cheti cha kuzaliwa, 
2.Kitambulisho cha Uzanzibari na
3. Cheti cha kumalizia masomo 

4. Maombi yote yaandikwe kwa mkono na yaelekezwe kwa Katibu  Mtendaji Kamisheni ya Wakf na Mali ya Amana Zanzibar. Tarehe  ya mwisho ya kupokea maombi hayo ni tarehe  20/07/2016. 

Ahsanteni.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.