Baada ya Kukamilika kwa kazi ya Uwekaji wa Raba ya kukimbilia
katika uwanja wa michezo Gombani Kisiwani Pemba, pichani ni muonekano wa mpya
wa uwanja huo baada ya wataalamu kutoka kampuni ya Guangzhou Jrage Athletic Facilities Co.LTD ya
nchini China, kukamilisha kazi hiyo.
Wataalamukutoka kampuni ya Guangzhou Jrage Athletic Facilities Co.LTD ya nchini China,
wakiwa katika hatua za mwisho kukamilisha kazi ya Uwekaji wa Tatani katika
uwanja wa gombani, pichani wataalamu hao wakiweka alama katika njia kwa
wanariadha ndani ya uwanja huo.
(Picha na
Abdi Suleiman.Pemba)
Na Abdi
Suleiman, Pemba.
KAZI ya Uwekaji wa Mpira wa
kukimbilia (Tatani) katika uwanja wa michezo Gombani, iiliyokuwa ikifanywa na
wataalamu kutoka kampuni ya Guangzhou Jrage Athletic Facilities Co.LTD ya
nchini China, imeshakamilika kwa asilimia 99.9.
Kazi
hiyo iliyokadiriwa kuchukuwa muda wa siku 40 hadi kukamilika kwake, lakini
wataalamu hao kutoka China wamelazimika kuifanya kazi hiyo kwa ufanisi zaidi.
Wataalamu
hao waliwasili kisiwani Pemba katikati ya Mwezi wa Juni mwaka huu, huku kazi
hiyo ya uwekaji wa tatani wakianza Juni 25, kwa kuweka sawa vifaa vyao, huku
hatua ya awali ya uwekaji wa raba hiyo ikianza Juni 29.
Mwandishi
wa habari hizi alifika katika uwanja huo wa michezo na kushuhudia wataalamu
hao, wakiwa katika hatua za mwisho katika uwekaji wa nambari kwenye njia za
kukimbilia wanariadha.
Akizungumza
na mwandishi wa habari hizi Afisa Mdhamini wa Wizara ya Habari, Utalii,
Utamaduni na Michezo Pemba, Khatib Juma Mjaja alisema kwa sasa kazi zilizobalia
ni ndogo ndogo lakini kwa asilimia 99.9 kazi hiyo imeshakamilika.
Alisema
wataalamu hao wamejitahidi kufanya kazi kwa umakini zaidi, ili kuhakikisha kazi
hiyo inakamilika kwa wakati, licha ya kukumbana na changamoto ya Mvua iliyokuwa
ikisitisha ufanyaji wao wa kazi.
Aliwataka
mashabiki wa mpira wa miguu kisiwani Pemba, kuendelea kuwa wastahamilivu katika
kipindi hicho ambacho uwanja uko katika hatua za matengenezo.
“Wanamichezo
endeleeni kuwa na uvimilivu mambo mazuri hayahitaji haraka, matumaini yenu
yamefikia na endeleeni kuwa wavumilivu mutarudi katika uwanja wenu”alisema.
Nao
wapenzi wa mipira wa miguu Kisiwani Pemba, waliokuwa wakifuatilia kazi hiyo ya
uwekaji wa tatani hiyo, waliishukuru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa
kuufanya uwanja huo kuwa wa kisasa zaidi.
Walisema
kukamilika kwa kazi hiyo basi ni moja ya hatua kubwa ya kuutangaza zaidi Uwanja
huo, kitaifa na kimataifa kwani vilabu mbali mbali vikubwa vitajitokeza
kuhitaji kufanya mazoezi kiwanjani hapo.
Omara
Ali Khamis aliyomba Serikali baada ya kumaliza kazi ya Uwekaji wa Tatan, kuuangalia
katika sehemu za majukwani, skoobodi na pamoja na paa la uwanja huo.
Alisema
pindi sehemu hizo pindi zikifanyiwa marekebisho basi uwanja huo utaweza kuwa
uwanja wa kisasa zaid, kwani baada ya uwekaji wa tatani umeweza kubadilika
pia.
“Tunapaswa kuishukuru Serikali yetu katika hatua kubwa iliyopitia, hili ni jambo la
kuwapongeza viongozi wa Serikali na Wizara ya Habari kwa kazi kubwa waliyofikia
ya uwekaji war aba hiyo”alisema.
Amini
Yussuf Khalfani alisema sasa matumaini ya wanamichezo wa kisiwa Cha Pemba,
yamerudi upya baada ya kazi ya uwekaji wa tatani kukamilikwa kwa asilimia
kubwa.
No comments:
Post a Comment