Habari za Punde

Waziri wa Fedha na Mipango Zanzibar Atembelea Mradi wa ZSSF Mnara wa Kumbukumbu ya Mapinduzi Michenzani Zanzibar.

Waziri wa Fedha na Mipango Zanzibar Mhe Dk Khalid Salum akisalimiana na Viongozi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar wakati wa ziara yake kutembelea Taasisi hiyo ilioko Chini ya Wizara ya Fedha na Mipango kuona maendeleo ya Mradi huo wa Mnara wa Kumbukumbu ya Mapinduzi ya Zanzibar ulioko Michezani Kisonge.
Waziri wa Fedha Dk Khalid Salum akisalimiana na Maofisa wa ZSSF alipowasili katika viwanja vya Mnara wa Kumbukumbu ya Mapinduzi ya Zanzibar Michezani akiwa katika ziara yake kutembelea Taasisi zilizopo chini ya Wizara ya Fedha na Mipango Zanzibar.
Waziri wa Fedha Zanzibar akielekea katika Mnara huo kuaza ziara yake kuangalia kumbukumbu ya Mapinduzi ya Zanzibar katika Mnara huo.


















No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.