Habari za Punde

CP.Kombo Awahakikishia Wananchi Usalama Siku ya Uchaguzi Mkuu Oktoba 2025 Zanzibar

Jeshi la Polisi limewataka wananchi kutokuwa na hofu ya ulinzi na usalama wao siku ya uchaguzi Oktoba 29, 2025 na limewasihi wakapige kura na limewahakikishia kuwa hakutakuwa na changamoto za kiusalama.

Akizungumza na Waandishi wa Habari Kamishna wa Polisi Zanzibar CP Kombo Khamis Kombo leo Oktoba 24, 2025  mazungumzo hayo yaliyofanyika Makao Makuu ya Polisi Kamisheni ya Zanzibar amesema Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na vikosi vyengine vya ulinzi na usalama limejipanga na limeweka mikakati ya kuimarisha ulinzi wakati wa uchaguzi na baada ya uchaguzi.

Amesisitiza Jeshi la Polisi litawachukulia hatua kwa mujibu wa sheria na halitakubali, halitamvumilia mtu au kikundi kitakachojaribu kuchochea ghasia, Kuhamasisha maandamano haramu au Kuwashawishi wananchi kuvunja sheria.

Kitengo cha Habari

Makao Makuu ya Polisi

Kamisheni ya Zanzibar.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.