Habari za Punde

Wizara ya Elimu yatakiwa kukagua mitaala ya skuli binafsi ili iende sambamba na skuli za serikali

NA  TAKDIR ALI.            MAELEZO .                    23-09-2016.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Muhammed Shein ameitaka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar kuifanyia ukaguzi mitaala ya Skuli za binafsi ili kwenda sambamba na mitaala ya  Skuli za Serikali.

Hayo ameyasema leo huko Uwanja wa Amani mjini Zanzibar wakati akihutubia wananchi  katika maadhimisho ya miaka 52 ya elimu bila malipo.

Amesema mitala ya skuli za binafsi haiendi sambamba na ile ya serikali kitu ambacho hakipaswi ,hivyo amesema  ikohaja ya Wizara ya elimu namafunzo ya amali Zanzibar kushirikiana katika kuangalia mitaala miataala hiyo ya ufundishaji  ili iende sambamba  na skuli za serikali.

Aidha amesema  mashirikiano ya pamoja yapande hizo mbili yatapelekea wanafunzi kufanya vizuri katika mitihani yao ya majaribio na ile ya mwisho wa mwaka.

Dkt. Shein amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imejipanga vyema katika kuhakikisha kwamba  inakabiliana na changamoto mbalmbali  zinazoikabili sekta ya elimu hapa Zanzibar ili kuhakikisha inafikia dhana ya Raisi wa kwanza wa Zanzibar Marehemu Mzee Abeid Amani Karume alioitangaza Elimu bila malipo  mwaka 1964.

Akiwazungumzia Wazazi juu ya suala zima laelimu kumpatia mtotoDkt. Ali Mohamed Shein amesema suala la elimu kwa mtoto hali mlazimu mwalimu pekeyake bali ni jambo la wote  ambalo linahitaji ushirikiano kati ya mwalimu wazazi na wanafunzi.

Amesema wasiachiwe walimu pekeyao kufundisha na kuwaongoza bali wae na ushirikiano wa pamoja.

Pamoja na hayo  Dkt.Ali Mohamed Shein alisema kabla ya Mapinduzi ya Mwaka1964  ilimu Zanzibar ilikuwa ikitolewa kwa misingi ya ubaguzi kituambacho kiliwafanya wonyonge kuikosa hakihiyo ya elimu  kitu ambacho  kwa sasa Zanzibar imepiga hatua kubwa mbele kwani upatikanaji wa elimu ni wa kila mmoja ambae kafikia umri wa kwenda skuli.

Ameseama haki hiyo sasa imefikiwa kukua nakwasaa kua na vyuo vikuu vitatu kwa ujumla wake mbapo kwa kiasi ya miaka 20 iliopita Zanzibar haikuwa na hata chuo kikuu kimoja na kupelekea wanaotaka kusoma kuenda nje ya Tanzania.

IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIBAR.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.