Habari za Punde

HAFLA MCHAPALO YA MIAKA 71 YA UMOJA WA MATAIFA YAFANA JIJINI DAR

Ziafuatazo ni picha za hafla mchapalo (Cocktail Party) ya kukata na shoka ya kusheherekea miaka 71 ya Umoja wa Mataifa tangu ulipoanzishwa iliyofanyika nyumbani kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez jijini Dar es Salaam ambapo mgeni rasmi alikuwa Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni na kuhudhuriwa na wageni mbalimbali mashuhuri kutoka taasisi mbalimbali za serikali, binafsi pamoja na mabalozi wa nchi mbalimbali.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akitoa salamu za Umoja wa Mataifa katika hafla mchapalo ya kusheherekea miaka 71 ya umoja huo tangu kuanzishwa kwake kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (hayupo pichani) kuzungumza na wageni waalikwa.
Mgeni rasmi Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akizungumza kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika hafla mchapalo ya kusheherekea miaka 71 ya Umoja wa Mataifa iliyofanyika nyumbani kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez (kulia) jijini Dar es Salaam.
Mgeni rasmi Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez wakigonga 'cheers' ya kutakiana kheri na afya njema katika hafla mchapalo ya kusheherekea miaka 71 ya Umoja wa Mataifa iliyofanyika Oktoba 24, 2016 jijini Dar es Salaam.
Mgeni rasmi Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez baada ya kugonga glass.
Shamra shamra za miaka 71 ya Umoja wa Mataifa zikiendelea jukwaa kuu.
Mgeni rasmi Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (katikati), Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez (kulia) pamoja na Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa wa Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Celestine Mushy (kushoto) wakitazama 'documentary' fupi kwenye hafla hiyo.
Mgeni rasmi Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (katikati) akibadilishana mawazo na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez (kulia) pamoja na Balozi wa Japan nchini Tanzania, Masaharu Yoshida.
MC wa hafla mchapalo ya miaka 71 ya Umoja wa Mataifa, Edgar Kiliba kutoka ofisi ya Mkuu wa Umoja wa Mataifa akiendesha hafla hiyo.
Wafanyakazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa wakibadilishana mawazo Anthony Rutabanzibwa (kushoto) na Amon Manyama katika hafla hiyo.
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP) nchini, Awa Dabo (katikati) kwenye hafla mchapalo ya kusheherekea miaka 71 ya Umoja wa Mataifa tangu kuanzishwa kwake.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Emslies Travel Ltd. Jaffer Hirji (kushoto) wakati wa hafla mchapalo ya kusheherekea miaka 71 ya Umoja wa Mataifa tangu kuanzishwa kwake.
Baadhi ya wageni waalikwa na waheshimiwa mabalozi wakibadilishana mawazo kwenye hafla hiyo.

Mtaalamu wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) nchini, Hoyce Temu (kulia) akiwa na baadhi ya wafanyakazi wenzake na wageni waalikwa kwenye hafla hiyo.
Picha juu na chini ni baadhi ya wageni waalikwa na wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa.






Nguse Nyerere akiwa na baadhi ya Maafisa wenzake wa Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki katika hafla mchapalo ya kusheherekea miaka 71 ya Umoja wa Mataifa.
Edgar Kiliba (katikati) wa ofisi ya Mkuu wa Umoja wa Mataifa akibadilishana mawazo na baadhi ya wageni waalikwa kwenye hafla mchapalo ya kusheherekea miaka 71 ya Umoja wa Mataifa iliyofanyika Oktoba 24, 2016 jijini Dar es Salaam.
Wageni waalikwa wakibadilishana mawazo.
Baadhi ya wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa katika picha ya pamoja.

Baadhi ya Maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki katika picha ya pamoja.
Wafanyakazi wa Ofisi ya Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Edgar Kiliba na Beatrice Mkiramweni katika picha ya pamoja.

Baadhi ya madereva wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa katika picha ya pamoja kwenye hafla hiyo.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez katika picha ya pamoja na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angeline Mabula (Mb) katika hafla ya kushehereka miaka 71 ya Umoja wa Mataifa iliyofanyika Oktoba 24, 2016 jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.