JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
OFISI
YA RAIS
TAWALA
ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA
|
||
![]() |
||
![]() |
Mkurugenzi wa Jiji,
20 Barabara ya Boma,
|
|
Simu:
Nukushi:
|
+255 27 2548072/2503494 (Director)
+255 27 2544330 (General)
+255 27 2545768
|
S. L. P. 3013,
23101 ARUSHA,
Tovuti: www.arushacc.go.tz
|
Unapojibu tafadhali taja:
|
||
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
Mkurugenzi
wa Halmashauri ya Jiji la Arusha ndugu
Athuman J. Kihamia anapenda kukanusha na
kutoa
ufafanuzi juu ya taarifa iliyosambazwa kwenye mitandao ya
kijamii kuhusu
matumizi ya mafuta lita 1900. Halmashauri
ya Jiji la Arusha ina jumla ya Idara
13 na Vitengo 5. Idara ni
Utawala, ujenzi, Fedha, Elimu Msingi, Elimu
Sekondari,
Maendeleo ya Jamii, Afya, Usafishaji na Mazingira,
Mipango miji,
Mipango Takwimu na Ufuatiliaji na Maji.
Vitengo ni Ugavi, Ukaguzi wa Ndani, Sheria na Uchaguzi.
Katika Idara zote kuna
jumla ya magari 48 mitambo 5 na
wastani wa matumizi ya mafuta kwa Idara zote ni
lita 18,900
kwa mwezi na Idara zenye matumizi makubwa ni ujenzi na
usafishaji
na mazingira hii inatokana na Idara hizi kutumia
idadi kubwa ya malori na
mitambo katika kutekeleza
shughuli zake. Mafuta yanaweza kununuliwa kwenye vituo
binafsi endapo itatokea dharura na GPSA inakosa mafuta na
manunuzi yatafanywa
kwa kuzingatia bei isiyozidi viwango
vya GPSA.
Baadhi
ya watu wasiokuwa na nia njema wanasambaza
taarifa hizo katika mitandao ya kijamii kutokana na juhudi
mbalimbali
ambazo Mkurugenzi amekuwa akizifanya za
kutatua kero mbalimbali kwa kubana
matumizi yasiyokuwa
ya lazima zikiwemo posho mbalimbali za watumishi na
Waheshimiwa Madiwani. Fedha nyingi huelekezwa katika
huduma mbalimbali za jamii
kama vile afya na elimu.
Hata hivyo kumekuwepo baadhi ya watu wasiokuwa
waaminifu ambao wamejipanga kuchafua kila jambo jema
linalofanywa na Mkurugenzi
wa Jiji nia yao kuu ikiwa ni
kumtoa kwenye lengo kuu la kuwahudumia wananchi
bila
ubaguzi wa aina yoyote, kusimamia miradi ya maendeleo
na matumizi ya fedha
zinazotokana na kodi za wananchi na ruzuku toka Serikali Kuu zilizokuwa
zikitumika kinyume na utaratibu.
Aidha
Mkurugenzi Kihamia amekuwa akipokea
jumbe za
vitisho na matusi kutoka kwa baadhi ya Madiwani lengo
likiwa ni
kudhoofisha juhudi anazozifanya za kuliweka Jiji
katika mstari.
Tangu
Mkurugenzi Kihamia alipoteuliwa amekuwa
akisisitiza kufuatwa kwa kanuni, sheria, taratibu na
miongozo na kuwachukulia
hatua wale wote waliokwenda
kinyume na utaratibu ikiwepo kurejeshwa posho
zinazolipwa kinyume na taratibu kwa Madiwani wa
Halmashauri ya Jiji la Arusha
na kufuta posho zisizokuwa
za lazima zilizokuwa zikilipwa kwa Maafisa
mbalimbali wa Jiji. Pia anatoa rai kwa watumishi wa Jiji wenye tabia yakutoa
nyaraka za Serikali kinyume na sheria na kusambazwa katika mitandao ya jamii
waache tabia hiyo kwani kosa la jinai na atakayegundulika atawajibika kwa mujibu wa sheria zilizopo. Ndugu
Kihamia ameahidi kuwa kumchafua katika mitandao ya kijamii hakutapunguza
dhamira yake ya kuwahudumia wananchi kwa weledi na uadilifu kwa kutenda
haki bila kumwonea mtu yeyote.
Tangu
alipofika Jiji la Arusha mwezi Julai 2016 Mkurugenzi
hajawahi kuidhinisha
mafuta, wala posho kwa ofisi ya
Mkuu wa Wilaya, wala kwa Mkuu wa Mkoa ambazo hazikuhusiani
na shughuli za Halmashauri ya Jiji la Arusha.
Hivyo
wananchi wanaombwa kupuuza taarifa hizo
kwani
hazina ukweli wowote na zina lengo la kumchafua
Mkurugenzi huyu.
Frank
R. Sanga
Afisa Tawala,
Halmashauri ya Jiji
Arusha.
05
Oktoba 2016
No comments:
Post a Comment