Habari za Punde

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe Riziko Pembe Afungua Mkutano wa Kimataifa wa Nchi za Visiwa Zilizoko Katika Mradi wa Eco Schools

Na.Kauthar Abdalla
Waziri ya elimu na mafunzo ya amali Zanzibar imesema itahakikisha ushirikiano zaidi unatolewa baina ya walimu na wadau katika mradi wa ikolijia maskulini (Eco schools) ili kufikia lengo lililokusudiwa.
Waziri wa elimu na mafunzo ya amali Zanzibar, Riziki Pembe Juma aliyasema hayo wakati wa ufunguzi wa mkutano wa tatu wa kimataifa wa nchi za visiwa duniani zilizomo kwenye mradi wa "Eco schools".
Aidha alisema ushirikiano huo atahakikisha unatolewa katika sekta za umma na  binafsi ili kila moja iwe na mchango katika mradi huo.
Alisema Wizara pia itashirikiana na wadau hao ili kuhakikisha program inapata wataalam na vifaa vinavyostahili kwani jukumu la kulinda mazingira ni la wote.
Alifahamisha kuwa programu ya Eco ina lengo la kuwawezesha wanafunzi, vijana na watoto kuwa na wajibu wa kuyaenzi Mazingira.
Nae Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maendeleo ya Vijana Elimu na Mazingira, (ZAYEDESA) mama Shadya Karume alisema ipo haja kwa walimu wa maskuli mbali mbali kuubeba mradi huo hasa skuli za Serikali kwa kuwaelimisha wanafunzi wayatunze mazingira ili itunzwe hali  ya hewa na ardhi ya nchi hii.
Alisema endapo mazingira yatatunzwa, nchi itakuwa na uwezo wa kuzalisha chakula hata katika maeneo ya skuli kwa kupanda vyakula kwa kuwa mazingira ndio sehemu ya maisha.
Hata hivyo Mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya kusimamia mazingira, (ZEMA) Sheha Mjaja Juma alisema suala la uhifadhi wa mazingira linafanana na nchi mbali mbali duniani hasa suala la udhibiti wa taka.
Sambamba na hayo alisema changamoto kubwa katika mazingira ni uchukuaji mali asili zisizorejesheka kutokana na uelewa mdogo wa jamii.

Mradi wa Ikolojia katika skuli za ukanda wa bahari ya Hindi maarufu kama "Eco Schools" unaratibiwa na Kamisheni ya Bahari ya Hindi (IOC) chini ya ufadhili wa Jumuiya ya Ulaya (EU), uliletwa nchini na Wizara ya Ardhi Maji Nishari na Mazingira nakuratibiwa na Jumuiya ya Mandeleo ya Vijana, Elimu na Mazingira, Zanzibar (ZAYEDESA) chini ya utekelezaji wa kamati ya kitaifa ya ZNSC iliyozishirikisha taasisi mbalimbali za umma na binafsi kwa ushirikiano na Wiraza ya Elimu na Mafunzo ya Amali, Zanzibar.


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.