Habari za Punde

Tanzania na Uturuki zasaini mikataba tisa ya maendeleo

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya mazungumzo na mgeni wake Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan (kulia) Ikulu leo jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya mazungumzo na mwenyeji wake Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli (hayupo pichani) Ikulu leo jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan akikagua gwaride mara baada ya kupokelewa na mwenyeji wake Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli (hayupo pichani) Ikulu jijini Dar es Salaam leo.

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan akiteta jambo na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majali (katikati) na Katibu Mkuu Kiongozi Mhandisi Balozi John Kijazi.
 Baadhi ya viongozi wa Serikali ya Jamhuri ya Miuungano wa Tanzania (waliokaa upande wa kulia) wakiweka saini katika mikataba na wawakilishi kutoka Serikali ya Uturuki leo jijini Dar es Salaam. Jumla ya mikataba tisa imetiwa saini, ikiwemo ushirikiano wa kimaendeleo.
 Waziri wa Fedha na Mipango wa Serikali ya Tanzania akibadilishana hati ya makubaliano na Waziri wa Fedha wa Uturuki leo jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) Dkt. Ayoub Ryoba akibadilishana hati ya makubaliano na mwakilishi wa Serikali ya Uturuki leo jijini Dar es Salaam.
  Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Augustine Mahiga  akibadilishana hati ya makubaliano na Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki leo jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan akiwapungia mkono wakazi wa jiji la Dar es Salaam waliofika kumlaki katika viwanja vya Ikulu leo.Kushoto kwake ni Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.
 Baadhi ya wananchi wakimlaki Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan alipowasili katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam leo. Rais huyo yupo nchini kwa ziara ya kikazi ya siku moja ambapo katika ziara hiyo Tanzania na Uturuki wameingia makubaliano katika mikataba tisa kwa lengo la kushirikiana na kusaidiana.
 Baadhi ya wageni walioambatana na Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan wakiingia katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam leo.
 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Moses Nnauye akiteta jambo na Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Harrison Mwakyembe walipokuta wakati wa ugeni wa Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan( hayupo pichani) leo jijini Dar es Salaam.
 Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akiwa ndani ya gari na mgeni wake Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan mara baada ya kumaliza mazungumzo Ikulu jijini la Dar es Salaam leo.
 Rais Dkt. John Pombe Joseph Maguli na mgeni wake Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan (walioshikana mikono) wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Mawaziri na viongozi kutoka Serikali za Tanzania na Uturuki leo jijini Dar es Salaam.

Picha na: Frank Shija – MAELEZO.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.