Habari za Punde

Rais wa Hoteli za Marriott Mashariki ya Kati na Afrika Atembelea Kisiwa cha Unguja Zanzibar na Kuzungumza na Mkurugenzi PennyRoyal

 

Marriott International Inc.ni kampuni ya Kimarekani inayomiliki hoteli nyingi za kimataifi katika kila pande ya dunia.Katika jitihada za kuongeza umaarufu wake,mwezi Septemba mwaka 2016 Marriott International Inc., ilinunua Hoteli za Star wood kwa gharama ya dola za Kimarekani bilioni kumi na tatu.

Pia mwaka 2014 Marriott International Inc ilifanikiwa kununua Protea Hospitality Group toka Afrika Kusini kwa dharama za dola za Kimarekani bilioni mbili.

Kwa manunuzi hayo Marriott International Inc., imekuwa ndio mmiliki mkubwa kuliko wote duniani ikiwa na jumla ya vyumba vya kulala wageni milioni moja nukta moja (1.1m) duniani kote.

Marriott International Inc. kwa sasa ipo katika mazungumzo ya mwisho na Pennyroyal Gibraltar Ltd kuhusu ujenzi wa Hotel ya Ritz Carlton Zanzibar ambayo itakua ndani ya Zanzibar Amber Resort.

Rais wa hoteli za Marriott Mashariki ya Kati na Afrika Bwana.Alex Kyriakidis ametembelea kisiwa cha Unguja na kukutana na wadau wa sekta ya utalii pamoja na viongozi wa serikali ya Zanzibar ili kujionea mazingira na kupata uelewa wa jinsi mradi huu utakavyoendelezwa hapa Zanzibar . 

Ni metegemeo yetu kuwa ujenzi wa Hoteli ya Ritz Carlton utachochea ongezeko la watalii ndani ya kisiwa cha Zanzibar na kukuza uchumi wake kwa ujumla.’ alisema Bw. Kyriakidis.

Ritz Carlton, ambayo inamilikiwa na Marriot International Inc.inamiliki hoteli moja tu barani Afrika iliyomo Cairo- Misri, na inategemea kuongeza matawi yake kisiwani Zanzibar kupitia Zanzibar Amber Resort. Ritz Carlton Zanzibar Hotel itajengwa katika usanifu wa kipekee kwenye eneo la ufukwe wa Bahari ya Hindi kaskazini mashariki mwa kisiwa hicho.

Bwana Alex Kyriakidi alisema ‘Ritz Carlton inafurahi kuingia ubia na Zanzibar Amber Resort 
katika harakati za kupanua wigo wake barani Afrika na kuleta uzoefu wake wa miaka mingi kwenye fani ya hoteli ndani ya Zanzibar. Ritz Carlton inaamini kuwa Zanzibar inauwezo mkubwa wa kukuza uchumi wake kupitia utalii,na nifuraha kubwa katika miongoni mwa kampuni inayochochea na kusaidia ukuwaji huo.’


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.