Habari za Punde

Tukio la Ajali Barabara ya Rahaleo Unguja.

Wananchi wa eneo la rahaleo wakiagalia ajali ya gari nnne zilizopata ajali katika makutano ya barabara ya rahaleo. Ajali hiyo imesababishwa na gari ndogo yenya namba za usajili Z 987 AB iliokatisha katika katikati ya barabara ya kwenda rahaleo studio na kupata ajali kwa kugongwa na gari ya daladala yenye namba za usajili Z 970 AN  daladala ya njia ya kinunu. gari hiyo ndogo na kusababisha kuzigonga gari mbili zilizopaki kando ya barabara hiyo. Katika ajali hiyo hakuna Mtu aliyejeruhiwa.  
Wananchi wakiagalia ajali hiyo iliyosababishwa na gari ndogo. baada ya kukatisha kuingia njia kuu.ikitokea katika mkunazi. 
 Gari iliyosababisha ajali hiyo ikiwa kando ya barabara hiyo.
 Waananchi wakiagalia gari iliyogonga gari nyengine iliokuwa kando barabara hiyo.




No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.