Habari za Punde

Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanawema Shein, Ameutaka Uongozi wa Taasisi ya Zanzibalicious Women Group Kuongeza Kasi.

STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar                                                                                                          26.03.2017
---
MKE wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein ameutaka uongozi wa Taasisi ya “Zanzibarlicious Women Group” kuongeza kasi ya kuendeleza shughuli zao kwa kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Taasisi nyengine katika kupambana na vitendo vya udhalilishaji wanawake na watoto.

Mama Shein aliyasema hayo katika hotuba yake aliyoitoa katika hafla ya muendelezo wa Siku ya Wanawake duniani, hafla iliyofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Hilton Double Tree, Shangani mjini Zanzibar.

Katika hotuba yake hiyo, Mama Shein alisema kuwa ni dhahiri kwamba jitihada za kuwasaidia wanawake wapate uwezo zaidi wa kufanya shughuli zaidi za kujiongezea kipato haziwezi kufanikiwa iwapo wataishi na hofu ya kufanyiwa vitendo udhalilishaji wao aau watoto wao.

Hivyo Mama Shein alisema kuwa taasisi hiyo ni vyema ikawa na mikakati madhubuti na kuungana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katikakupambana na vita hivyo.

Kwa kujua changamoto zinazowakabili watoto katika maisha yao Mama Shein alaisema kuwa jitihada za makusudi zinahitajika ili wasipoteze matarajio waliyonayo na kuwataka wazazi waendelee kuwaongoza, kuwafunza maadili mema kwa mujibu wa mafunzo ya dini silka na utamaduni wa Kizanzibari huku akiwataka watoto kuongeza bidii katika masomo yao.

Aliongeza kuwa jambo la kutia moyo ni kuwa Taasisi hii pia, inashughulikia ustawi wa watoto na hasa watoto wa kike na kueleza furaha yake kwa Taasisi hiyo imelitambua jukumunhilo wakiwa wanawake kwa kuwashughulikia waoto wao katika masuala mbali mbali yanayohusu ustawi wao.

Mama Shein alitoa wito kwa Taasisi hiyo kutokata tama kutokana na kukabiliwa na changamoto mbali mbali katika majukumu yao na kuwataka kuzitumia changamoto hizo kuwa ni fursa za kuwaletea maendeleo.

Alisekama kuwa jitihada za taasisi hiyo zinakwenda sambamba na mipango ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar chini ya uongozi wa Rais Dk. Ali Mohamed Shein katika kuwawezesha wanawake waliojiajiri wenyewe kwa lengo la kujiongeze kipato.

Sambamba na hayo, Mama Shein alitoa pongezi kwa Taasisi hiyo kwa kazi nzuri ambayo imekuwa ikiifanya tangu ilipoanzishwa na kuwataka kutambua kwamba Serikali inathamini sana kazi nzuri inayofanywa na Taasisi hiyo katika jamii.

Risala ya Taasisi hiyo ya wanawake iliyoanzishwa mwaka 2011 na kusajiliwa rasmi mwaka 2013 ilisomwa na Mtunza nidhamu wa Taasisi hiyo Shangwe Ramadhan Yussuf,ambayo ilieleza nia yake ikiwa ni kumuendeleza na kumuwezesha mwanamke kiuchumi, kijamii na ,imwenendo.

Aidha, risala hiyo ilieleza, changamoto, mafanikio na malengo ya Taasisi hiyo ambapo miongoni mwa malengo yake ni pamoja na kutoa eleimu ya ujasiriamali kwa vikundi mbalimbali vya wanawake na kuwawezesha kubuni biashara ndoho ndogo na jinsi ya kuweza kutafuta mitaji kutoka taasisi mbali mbali za kitaifa.

Mapema Waziri wa Kazi, Uwezeshajai Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto, Moudline Castico alitia pongezi kwa Taasisi hiyo na kueleza kuwa Wizara yake iko tayari kuendelea kutoa ushirikiano na Taasisi hiyo na nyenginezo zenye malengo kama hayo.

Pamoja na hayo, Waziri huiyo alitumia fursa hiyo kutoa pongezi kwa Dk. Shein kwa kutimiza mwaka mmoja tokea kuingia madarakani katika awamu ya pili ndani ya Serikali ya Awamu ya Saba kutokana na ushisndi wa kishindo alioupata katika uchaguzi uliopita.

Nae Mlezi wa Taasisi hiyo ambaye pia, ni Waziri wa Afya Mahmoud Thabit Kiombo alieleza historuia fupi ya Taasisi hiyo na kupongeza juhudi inazozifanya katika kufikia malengo yake na kusisitiza haja ya kuungwa mkono ili izidi kupata mafanikio zaidi.

Katika hafla hiyo michango ya harambee ilifanyika ambapo Mama Shein akiwa mgeni rasmi alichangia Tsh. Milioni moja pamoja na kugawa vyeti  maalum kwa watu maalum kwa juhudi zao za kuiunga mkono taasisi hiyo.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar

Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 
 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.