Kamishna wa Jeshi la Polisi Zanzibar, Hamdan Omar
Makame, akitoa taarifa za utekelezaji wa zoezi la kudhibiti Dawa za Kulevya
Visiwani humo kwa Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad
Masauni (kushoto), wakati wa ziara ya naibu waziri kufuatilia utekelezaji wa
zoezi la kudhibiti uingiaji wa dawa za kulevya Visiwani humo
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi
Hamad Masauni, akizungumza na Maafisa wa Idara ya Uhamiaji Zanzibar, wakati wa
ziara ya kukagua udhibiti wa uingiaji wa Dawa za Kulevya Visiwani humo, huku
akiagiza vyombo vya ulinzi na usalama kushirikiana kudhibiti madawa hayo ambayo
yanaharibu nguvu kazi ya Taifa
Mkuu wa Idara ya Uhamiaji anayesimamia Uwanja wa
Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani
Karume, Fulgenze Mutarasha, akitoa maelezo kwa Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni (wakwanza kushoto), juu ya hatua
zinazochukuliwa na Idara ya Uhamiaji na vyombo vingine vya Ulinzi na Usalama
kukabiliana na udhibiti wa uingiaji wa Dawa za Kulevya kiwanjani hapo.Wapili
kushoto ni Naibu Waziri Wizara ya
Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar,Mohamed
Ahmada Salumna anayefuatia ni Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Johari Masoud Sururu
Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya
Nchi,Mhandisi Hamad Masauni (kushoto), akisikiliza jinsi mifumo ya kudhibiti uingiaji haramu inavyofanya
kazi kutoka kwa Mkuu wa Idara ya Uhamiaji anayesimamia Uwanja wa Ndege wa Abeid Amani Karume, Fulgenze Mutarasha.Ziara
ya Naibu Waziri huyo ilikua na lengo la kukagua mifumo inayotumika kudhibiti
uingiaji wa Dawa za Kulevya
Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya
Nchi,Mhandisi Hamad Masauni, akitoa maelezo kwa watumishi wa Idara ya uhamiaji
waliopo Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume wakati wa ziara ya ukaguzi
wa mifumo ya kudhibiti uingiaji wa Dawa za Kulevya Visiwani Zanzibar
Naibu Waziri Wizara ya
Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni, akiteta jambo na Naibu Waziri
Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano wa Serikali ya Mapinduzi
Zanzibar,Mohamed Ahmada Salum wakati wa ziara ya ukaguzi wa mifumo ya kudhibiti
uingiaji wa Dawa za Kulevya katika Uwanja wa Ndege wa Sheikh Abeid Amani
Karume.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
IMEANDALIWA
NA KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI-WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
No comments:
Post a Comment